Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, March 27, 2014

KESI YA UAMSHO YAHAIRISHWA HADI JULIA 3






na harith subeit

zanzibar.

kesi inayowakabili viongozi wa jumuiya na taasisi zakiislam zanzibar imeakhirishwa hadi julai 3 mwaka huu ambapo imewekewa pingamizi na mkurugenzi wa mashtaka kuhusu dhamana iliyotolewa kwa washtakiwa hao.

mapema muendesha mashitaka kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashitaka dpp raya mselem aliwasilisha pingamizi ya kupinga uamuzi wa mahkama kuu kusikiliza ombi la dhamana ya watuhumiwa hao.

licha ya mahakama kuu kutoa dhamana kwa watuhumiwa bado upande wa mashtaka unapinga suala hilo na umeamua kukata rufaa ili washtakiwa warejeshwe tena rumande baada yakukaa ndani mwaka mmoja na miezi minne.

hata hivyo wakili wa upande wa utetezi abdalla juma ameiomba mahkama hiyo kuakhirisha shauri hilo hadi mahakama ya rufaa itakapokaa na kusikiliza rufaa hiyo.

hata hivyo jaji isack sepetu hakupingana na hoja hiyo.

watuhumiwa waliofika mahakamani leo ni pamoja na amiri mkuu wa jumuiya ya maimamu zanzibar samahatu sheikh farid hadi ahmed,amiri mkuu wa jumuiya ya uamsho na mihadhara yakiislam zanzibar fadhilatu sheikh mselem bin aly, naibu amiri wa jumuiya ya uamsho na mihadhara yakiislam zanzibar zanzibar al-ustadh azan khalid hamdan.

wengine ni katibu wa jumuiya ya uamsho na mihadhara yakiislam zanzibar al-ustadh abdalla saidi, maustadh mussa juma mussa, suleiman juma sleiman, khamis ali sleiman, hassan bakari sleiman, gharibu ahmada juma, na majaliwa fikirini majaliwa.

mashtaka waliosomewa washitakiwa hao ni kuharibu mali, uchochezi,ushawishi , kuhamasisha fujo na kosa la tatu ni kula njama ya kufanya kosa
kosa la nne likimkabili mshitakiwa namba nne al-ustadh azan khalid ambae anadaiwa kutoa maneno ya matusi kwa kamishna wa polisi vitendo vinaweza v kusababisha uvunjifu wa amani.

vitendo hivyo vinadaiwa kufanyika kati ya oktoba 17,18 na 19 mwaka ,2012 katika maeneo tofauti katika manispaa yaa mji wa zanziba ambapo washitakiwa hao wote wamekana makosa yote hayo.

viongozi hao walipewa dhamana na mahakama kuu ya zanzibar tarehe 27 mwezi wa pili mwaka huu baada yakutekeleza masharti yaliyowekwa.