Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, January 17, 2014

kesi inayowakabili viongozi wa harakati ya jumuiya na taasisi zakiislam zanzibar .






mahkama kuu vuga mjini zanzibar imeutaka upande wa mashtaka  kuwasilisha vielelezo na maelezo ya ushahidi vitakavyotumika  katika kesi inayowakabili viongozi wa  harakati ya jumuiya na taasisi zakiislam zanzibar .



jaji wa mahkama hiyo fatma hamid mahmoud ametoa ombi hilo alipokuwa akiendesha kesi  inayowakabili viongozi hao katika mahakam kuu vuga mjini zanzibar .



jaji huyo pia ameutaka upande wa mashtaka kuwasilisha kwa maandishi sababu za  kuzuiya dhamana ya  viongozi hao waliokaa rumande  kwa mwaka mmoja sasa.



hatua hiyo imekuja  baada ya mwendesha mashtaka wa serikali rashid abdalla kudai kuwa vielelezo vya ushahidi wa kesi hiyo tayari vimekamilia hivyo  ipangiwe tarehe nyengine ili kuwasilisha vielelezo vya mashahidi.



kwa upande wake wakili anaesimamia watuhumiwa wa kesi hiyo abdalla juma  ameiomba mahkama kupanga tarehe ya kusikilizwa  kwa kesi hiyo na vielelezo viwasilishwe mahkamani hapo kutokana na  ushahidi wa kesi hiyo kukamilika.



hata hivyo upande wa mashitaka haukuwa na pingamizi na na ombi hilo na  umedai kuwa unaiachia mahkama kuamua.



watuhumiwa katika kesi hiyo  ni   amiri mkuu wa jumuiya ya maimamu zanzibar samahatu sheikh farid hadi ahmed  mkaazi wa mbuyuni,amiri mkuu wa jumuiya ya uamsho na mihadhara yakiislam zanzibar fadhilatu sheikh mselem ali mselem  mkaazi wa kwamtipura, ustaddh mussa juma mussa  mkaazi wa makadara 

wengine ni  maustadh suleiman juma suleiman  mkaazi wa makadara, khamis ali suleiman mkaazi wa mwanakwerekwe, hassan bakar suleiman mkaazi wa tomondo, ghalib ahmada juma mkaazi wa mwanakwerekwe ,katibu wa jumuiya ya uamsho na mihadhara yakiislam zanzibar  al-ustadh abdallah said mkaazi wa misufini na fikirini majaliwa fikirini.



mashtaka waliosomewa washitakiwa hao ni kuharibu mali,  uchochezi,ushawishi na kuhamasisha fujo na kosa la tatu ni kula njama ya kufanya kosa.



kosa la nne linamkabili mshitakiwa namba nne al-. naibu amiri wa jumuiya ya uamsho na mihadhara yakiislam zanzibar  al-ustadh azan khalid ( mkaazi wa mfenesini.



ustadh azan khalid hamdan anadaiwa kutoa maneno ya matusi kwa kamishna wa polisi vitendo vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani.



vitendo hivyo vinadaiwa   kufanyika kati ya oktoba 17,18 na 19 mwaka 2013 katika maeneo  mbali mbali katika manispaa ya mji wa zanzibar.



jaji fatma ameikhirisha kesi hiyo na kutaka upande wa mashitaka kuwasilisha vielelezo na maelezo ya kesi hiyo  kabla ya  januar 31 mwaka huu. 

Thursday, January 9, 2014

Abdiweli Mohamed, rais mpya wa Puntland, Somalia


Abdiweli Mohamed, rais mpya wa Puntland, Somalia
Dakta Abdiweli Mohamed Ali, Waziri Mkuu wa zamani wa Somalia leo amechaguliwa kuwa Rais wa eneo lenye mamlaka ya ndani la Puntland, baada ya kumshinda mpinzani wake Abdirahman Mohamed Mohamud kwa zaidi ya kura moja, katika uchaguzi huo uliojaa ushindani mkubwa.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Puntland, wabunge 66 wa eneo hilo waliochaguliwa na wakuu wa makabila mwezi uliopita, ndio wenye jukumu la kumchagua Rais wa eneo hilo lililoko kaskazini mashariki mwa Somalia.
Tume ya Uchaguzi ya Puntland ilipitisha majina ya wagombea 11 kati ya 15 waliojitokeza kuwania nafasi hiyo, katika eneo hilo lililojitangazia mamlaka ya ndani tokea 1998.
Dakta Abdiweli Mohamed Ali aliwahi kuhudumu nafasi ya Uwaziri Mkuu wa Somalia tangu mwaka 2009 hadi mwaka 2012. Inafaa kuashiria hapa kuwa, mapigano yaliyoanza mwaka 1991 nchini Somalia baada ya kuangushwa utawala wa Jenerali Muhammad Siad Barre, yalisababisha baadhi ya maeneo ya Somalia kujitangazia mamlaka ya ndani, kama Somaliland na Puntland. 

WFP yawapatia chakula wakimbizi wa ndani CAR


WFP yawapatia chakula wakimbizi wa ndani CAR
Shirika la Mpango wa ChakulalaUmoja wa Mataifa (WFP) limeanza tena kugawa chakula kwa familia za wakimbizi wa ndani ya nchi katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Taarifa ya WFP imesema chakula kitatolewa kwa watu wapatao 100,000 ambao wamepata hifadhi katika uwanja wa ndege wa Bangui, mjii mkuu wa nchi hiyo iliyokumbwa na vita vya ndani. Ugawaji huo umeanza tena baada ya kusitishwa kwa wiki tatu kutokana na hali ya usalama kwenye eneo hilo.  WFP inashirikiana na mashirika kadhaa ya Umoja wa Mataifa na mashirika yasiyo ya kiserikali pamoja na viongozi wa kijamii ili kuhakikisha mazingira yanaruhusu kusambaza msaada wa chakula na misaada mingine kwa wakimbizi wa ndani. Wananchi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati wanaituhumu Ufaransa ambayo ni mkoloni wa zamani wa nchi hiyo kuwa inachochea mapigano hasa uhasama baina ya Waislamu na Wakristo nchini humo. Jamhuri ya Afrika ya Kati ni nchi yenye umuhimu mkubwa kwa madola makubwa ulimwenguni kutokana na kuwa kwake katika kitovu cha bara la Afrika. Nchi hiyo inakodolewa jicho la tamaa na nchi kubwa duniani kutokana na utajiri mkubwa wa maliasili za madini kama almasi, urani na dhahabu.

Mapigano makali yaendelea nchini Sudan Kusini


Mapigano makali yaendelea nchini Sudan KusiniMapigano makali yanaripotiwa kuendelea kati ya wanajeshi wa serikali ya Sudan Kusini na waasi wanaoongozwa na makamu wa zamani wa rais Riek Machar.
Msemaji wa jeshi la Sudan Kusini Philip Aguer amesema siku ya Jumatano walipambana vikali na waasi katika kupigania udhibiti wa Bor, mji mkuu wa Jimbo la Jonglei. Aidha mapigano yanaripotiwa kuendelea katika jimbo lenye utajiri wa mafuta la Nile ya Juu. Msemaji wa waasi Youhani Musa Pauk amesema hakutakuwa na usitishaji mapigano hadi pale serikali ya Juba itakapowaachilia huru wanasiasa wapinzani ambao walitiwa mbaroni punde baada ya machafuko kuibuka wiki tatu zilizopita. Huku hayo yakijiri wapatanishi kutoka jumuiya ya kieneo ya IGAD wanasema mazungumzo baina ya pande hasimu yanaendelea vizuri na kwamba Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amesitiza kuwa mgogoro wa sasa ni wa kisiasa na kwamba anaunga mkono suluhisho la kisiasa. Machafuko nchini Sudan Kusini yalianza Disemba 15 katika mji mkuu Juba, pale wanajeshi wanaoaminika kuwa watiifu kwa Riek Machar, walipojaribu kuipindua serikali ya Rais Salva Kiir. Uhasama wa kisiasa nchini humo ulianza mwezi Julai mwaka jana baada ya Kiir kumfuta kazi Machar. Kiir ni kutoka kabila la Dinka ambalo ndilo lenye nguvu zaidi na Machar ni wa kabila la Nuer.