Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, January 9, 2014

WFP yawapatia chakula wakimbizi wa ndani CAR


WFP yawapatia chakula wakimbizi wa ndani CAR
Shirika la Mpango wa ChakulalaUmoja wa Mataifa (WFP) limeanza tena kugawa chakula kwa familia za wakimbizi wa ndani ya nchi katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Taarifa ya WFP imesema chakula kitatolewa kwa watu wapatao 100,000 ambao wamepata hifadhi katika uwanja wa ndege wa Bangui, mjii mkuu wa nchi hiyo iliyokumbwa na vita vya ndani. Ugawaji huo umeanza tena baada ya kusitishwa kwa wiki tatu kutokana na hali ya usalama kwenye eneo hilo.  WFP inashirikiana na mashirika kadhaa ya Umoja wa Mataifa na mashirika yasiyo ya kiserikali pamoja na viongozi wa kijamii ili kuhakikisha mazingira yanaruhusu kusambaza msaada wa chakula na misaada mingine kwa wakimbizi wa ndani. Wananchi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati wanaituhumu Ufaransa ambayo ni mkoloni wa zamani wa nchi hiyo kuwa inachochea mapigano hasa uhasama baina ya Waislamu na Wakristo nchini humo. Jamhuri ya Afrika ya Kati ni nchi yenye umuhimu mkubwa kwa madola makubwa ulimwenguni kutokana na kuwa kwake katika kitovu cha bara la Afrika. Nchi hiyo inakodolewa jicho la tamaa na nchi kubwa duniani kutokana na utajiri mkubwa wa maliasili za madini kama almasi, urani na dhahabu.

No comments:

Post a Comment