Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, February 12, 2013

Kenya yapinga uingiliaji wa madola ya kigeni


Kenya yapinga uingiliaji wa madola ya kigeni Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Kenya Sam Ongeri amelaani uingiliaji wa nchi za Ulaya katika masuala ya ndani ya nchi hiyo.
Ongeri amesema kuwa, wanadiplomasia wa nchi za Ulaya wanafanya njama za kuathiri matokeo ya uchaguzi ujao wa rais nchini humo. Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Kenya amesisitiza kuwa, matamshi ya wanadiplomasia wa nchi hizo kuhusiana na uchaguzi ujao wa rais nchini Kenya yanachochea anga ya kisiasa nchini humo.

Hivi karibuni Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga ambaye anawania nafasi ya urais kwa tiketi ya muungano wa CORD aliwataka wasimamizi wa uchaguzi kutoka Ulaya kufanya tathmini ya kina na  uhakika katika hatua za awali za uchaguzi mkuu wa Kenya. Uchaguzi mkuu wa nchi hiyo umepangwa kufanyika tarehe 4 Machi mwaka huu.

No comments:

Post a Comment