Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, February 1, 2013

Vita vya Ufaransa Mali: Haki za binaadmau zakiukwa



Wanajeshi wa Ufaransa nchini Mali 
Shirika la kutetea haki za binaadamu la Human Rights Watch limetaka uchunguzi ufanyike kuhusu vitendo vya ukiukwaji wa haki za binaadamu vinavyotendwa na vikosi vya kijeshi vinavyoongozwa na Ufaransa nchini Mali.
Mkurugenzi wa Human Rights Watch barani Afrika Tiseke Kasambala ametoa taarifa na kuvitaka vikosi vya Ufaransa kupunguza ukatili na mauaji ya raia Mali.
Ufaransa ilianzisha vita dhidi ya Mali karibu mwezi mmoja uliopita kwa kisingizio cha kupambana na magaidi kaskazini mwa nchi hiyo. Tayari wanajeshi kutoka Niger na Togo wameshajiunga na vikosi vya Ufaransa katika vita nchini Mali. Imearifiwa kuwa mji wa Gao sasa unadhibitiwa na vikosi vya Ufaransa baada ya kushikiliwa na waasi kwa muda wa miezi 10. Nchi zinazounga mkono vita vya Ufaransa nchini Mali ni pamoja na Marekani, Canada, Uingereza, Ubelgiji, Ujerumani na Denmark. Weledi wa mambo wanasema lengo la vita vya Mali ni kupora utajiri mkubwa wa mali asili nchini humo kama vile mafuta, dhahabu na madini ya urani.

No comments:

Post a Comment