Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, February 2, 2013

IRAN YAONYESHA NDEGE YAKE YA KIVITA QAHER-313



Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeonyesha ndege yake ya kivita iliyotengenezwa hapa nchini ambayo uwezo wake ni sawa na ndege ya kivita ya Marekani ya F/A 18. Ndege hiyo ya kivita yenye jina la Qaher-313 yaani mshindi imeonyeshwa katika marasimu yaliyofanyika leo Jumamosi na kuhudhuriwa na Meja Jenerali Ataollah Salehi Kamanda wa Jeshi la Iran, Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia Jenerali Ahmad Vahidi na Kamanda wa Jeshi la Anga la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Brigedia Jenerali Hassan Shah Safi katika maadhimisho ya Alfajiri Kumi katika kukumbuka ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu mwaka 1979. 

Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Iran amesema katika ufunguzi wa sherehe hizo kuwa ndege hiyo ya kivita ya Iran imebuniwa na kutengenezwa kikamilifu na wataalamu wa Iran.

No comments:

Post a Comment