Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, February 2, 2013

'Vikosi vya Ufaransa vitaondoka Mali kwa wakati'


'Vikosi vya Ufaransa vitaondoka Mali kwa wakati'
Rais Francois Hollande wa Ufaransa amesema vikosi vya nchi hiyo vitaendelea na operesheni zake huko kaskazini mwa Mali lakini vitakabidhi kwa wakati hatamu za uendeshaji operesheni hizo kwa vikosi vya askari wapatao 8,000 wa nchi za Afrika. Hollande ameyasema hayo leo alipokutana na vikosi vya Ufaransa huko Timbuktu wakati wa safari yake ya siku moja nchini Mali huku kukiwepo madai kwamba raia wa kawaida wameuawa kutokana na mashambulio ya anga ya Ufaransa sambamba na mauaji ya kikabila wakati wa operesheni hiyo ya kuingilia kijeshi huko kaskazini mwa Mali.
Kwa mujibu wa duru za habari hadi sasa malengo mawili ya operesheni ya kijeshi ya Ufaransa huko Mali yameshafikiwa ambayo ni kuwazuia waasi wasisonge mbele kuelekea kusini na kuikomboa miji iliyokuwa imetekwa na waasi hao. Hata hivyo lengo kuu la tatu kama lilivyoelezwa na Rais wa Ufaransa ambalo ni kurejesha udhibiti wa ardhi yote ya Mali kama taifa moja na chini ya uongozi wa serikali kuu bado halijafikiwa.

No comments:

Post a Comment