Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, February 12, 2013

‘Sudan Kusini inapanga kuvuruga amani ya Sudan’


‘Sudan Kusini inapanga kuvuruga amani ya Sudan’Chama cha Kongress ya Taifa kinachotawala nchini Sudan, kimefichua njama iliyoratibiwa na Sudan Kusini kwa kushirikiana na Marekani na utawala haramu wa Kizayuni, kwa ajili ya kuharibu hali ya amani nchini humo. Chama hicho kimefafanua kuwa, Sudan Kusini kwa kushirikiana na Marekani na utawala haramu wa Kizayuni inafanya njama ya kuzusha machafuko katika maeneo ya Kordofan Kusini na katika jimbo la Darfur kwa kuwaunga mkono wapinzani wa serikali ya Khartoum. Aidha chama hicho kimesisitiza kuwa, njama hiyo ina lengo la kuandaa uwanja kwa Marekani na utawala ghasibu wa Israel katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, kuituhumu Khartoum na hivyo kupelekea kuongezwa vikwazo dhidi ya Sudan.
Qutbi Al-Mahdi mkuu wa ofisi ya Chama cha Kongress ya Kitaifa nchini Sudan pia amesema kuwa, askari wanaoungwa mkono na Juba wanaendelea kutekeleza ajenda za madola ya kigeni ukiwemo utawala wa Kizayuni kwa lengo la kuvuruga usalama wa nchi hiyo.  

No comments:

Post a Comment