Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, February 12, 2013

Tanzania yang'ara maajabu saba ya Afrika


Tanzania yang'ara maajabu saba ya Afrika
Tanzania imepata tunzo tatu za maajabu saba ya Afrika kupitia vivutio vyake bora vya utalii vya Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Ngorongoro na Hifadhi ya Serengeti ambavyo viliongoza kwa kupata kura nyingi kuliko nchi nyingine yoyote.  Akitangaza matokeo hayo mjini Arusha kaskazini mwa Tanzania mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, mkuu wa taasisi iliyoandaa tunzo hiyo Dk. Phillip Imler wa Marekani, amesema, ushindi huo umetokana na kuwa Tanzania ina vivutio vya kipekee. Akielezea hifadhi ya taifa ya Serengeti, alisema kuwa ndiyo hifadhi ya kipekee iliyopata kura nyingi kutokana na tabia ya misafara ya wanyama wanaohama kwa msimu.
Naye Waziri Mkuu wa Tanznaia Mizengo Pinda ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo amesema kuwa nchi za Afrika zina vivutio vingi vya utalii na fursa kubwa ya kukuza pato kupitia utalii huo. Aidha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameongeza kuwa, anaamini kutokana na sifa ambayo Tanzania imeipata kupitia vivutio vyake hivyo vitatu itaendelea kuvitunza na kuhakikisha kuwa vinavutia zaidi watalii na kuongeza pato la taifa.

No comments:

Post a Comment