Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, October 31, 2012

Mugabe: Uchaguzi Mkuu utafanyika Machi mwakani



Mugabe: Uchaguzi Mkuu utafanyika Machi mwakani
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amesema kuwa lengo lake kuu ni kuendesha uchaguzi kote nchini humo ifikapo mwezi Machi mwakani kwa mujibu wa katiba mpya ya nchi hiyo. Mugabe amesema kuwa harakati zao zinapasa kusonga mbele licha ya mitazamo yao ya kisiasa kutofautiana. Mugabe ameyatamka hayo katika kikao kilichohudhuriwa pia na Morgan Tsvangirai Waziri Mkuu wa Zimbabwe na ambaye pia ni mpinzani wake mkuu wa kisiasa. Kamati ya katiba ya Zimbabwe imesaini rasimu ya mwisho ya katiba hiyo mpya na kuidhinishwa na karibu mirengo yote mikuu ya kisiasa na kiraia ya nchi hiyo, hata hivyo tarehe ya kufanyika kura ya maoni kuhusiana na katiba hiyo bado haijatangazwa. Kura ya maoni ndiyo itakayofungua njia ya kufanyika chaguzi zijazo za Rais na Bunge huko Zimbabwe.

Mfumuko wa bei wapungua Kenya


Mfumuko wa bei wapungua Kenya
Mfumuko wa bei Kenya umepungua kwa kiasi cha chini zaidi katika kipindi cha miezi 23 iliyopita na hivyo kuibua matumaini miongoni mwa wananchi.
Kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Kenya  (KNBS), pamoja na kuwepo ongezeko la bei ya mafuta ya petroli, mfumuko wa umeshuka hadi asilimia 4.14 mwezi Oktoba ikilinganishwa na asilimia 5.32 mwezi Septemba mwaka huu. Kiwango cha mfumuko wa bei Kenya sasa ni cha chini zaidi tokea Desemba mwaka 2010.
Katika taarifa  kaimu mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Kenya  Zachary Mwangi amesema kumeshuhudiwa kushuka bei ya vyakula kama vile sukuma wiki,mahindi, tomato na  karoti. Hatahivyo amesema kumeshuhudiwa ongezeko la bei ya baadhi ya bidhaa kama vile viazi, ndizi na nyama ya ng’ombe.
Weledi wa mambo wanasema mfumuko wa bei umepungua Kenya kutokana na ongezeko la uzalishaji wa vyakula, kupungua bei ya petrol kimataifa katika mizi iliyotnagulia na usimamizi bora ya kifedha.

'Mataifa yataendelea kwa kujitenga na Marekani'


'Mataifa yataendelea kwa kujitenga na Marekani' Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, ikiwa mataifa ya eneo la Mashariki ya Kati na mengineyo yatathubutu kutenga siku moja na kuitangaza kuwa ni siku ya kujibari na Marekani, basi bila ya shaka yoyote mataifa hayo yatakuwa yamepiga hatua kubwa ya kihistoria. Kiongozi Muadhamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ameyasema hayo Jumatano hii mjini Tehran alipokutana na maelfu ya wanachuo na wanafunzi tofauti katika kukaribia kwa tarehe 13 Aban sawa na tarehe 4 Novemba, ambayo hapa nchini Iran inahesabiwa kuwa ni siku ya taifa ya wanafunzi na kupambana na ubeberu wa kimataifa. Kiongozi Muadhamu amewataka viongozi na wakuu wa mihimili mitatu ya dola yaani serikali, bunge na mahakama nchini Iran, kufanya kazi kwa bidii na kwamba katika kipindi hiki wanatakiwa kuwa makini katika utendaji wa kazi zao na wajiepushe na masuala madogomadogo yanayoenezwa na makelele ya vyombo vya habari vya Wamagharibi.

The Best Muslim football Players In The World

Ricardo kaka convert to muslim (ISLAM) and his family

Muslim Football Stars

Lionel Messi Converts to Islam in this Ramadan لیونل میسی به اسلام مشرف شد

KOMBORA KALI LASHUSHWA NA LARIPUA MAREKANI

KOMBORA KUBWA LA HATARI ALILOLISHUHSA ALLAAH KWA NCHI YA MAREKANI, LINAENDELEA KUATHIRI NCHI HIYO KATIKA SEHEMU ZA NEW YORK STATE.
KOMBORA HILO AMBALO WAMAREKANI WAMELIPA JINA LA SANDY, LIMEHARIBU SEHEMU KADHAA ZA NEW YORK NA NGUVU YAKE KUINGIA KATIKA SEHEMU ZA KARIBU NA JIMBO HILO IKIWA NI PAMOJA NA CANADA.
SILAHA ZA ALLAAH HAZITUMII URENIUM, LAKINI UKALI WAKE NI MKUBWA KULIKO ULE WA MABOMU YANAYOTUMIWA NA MAREKANI AMBAYO HUTENGENEZWA KWA KUTUMIA CHEMICALI NA MADINI NYENGINE WANAZOZIJUA WAO.
TUNAISHAURI MAREKANI NA WATU WAKE KUMFAHAMU ALLAAH NA MTUME WAKE MUHAMMAD BADALA YA KUKAA NA KUSINGIZI KUWA HALI HIYO NI YA KAWAIDA IKIWA NI KUCHAFUKA KWA HALI YA HEWA.  WAMERAKANI LAZIMA WAFAHAMU KUWA MADHARA YANAYOWATOKEA KILA MARA NI MATOKEAO YA UADUI WAO KWA MTUME MUHAMMAD, HASA TUKIO LA HIVI KARIBUNI LA KUMKASHIFU MTUME WETU SAW, KWA KUTENGENEZA FILAMU NA VIKATUNI DHIDI YA MTUME MUHAMMAD SAW.
TUNATEGEMEA HALI HII ITAENDELEA KUTOKEA KILA MWAKA MPAKA PALE MAKAFIRI HAO WATAKAPOREJEA KWA ALLAAH NA KUMTAMBUA MTUME WA MWISHO WA MWENYWEZI MUNGU, MUHAMMAD SAW.

Tuesday, October 30, 2012

Ujumbe wa Bunge la Iran kuitembelea Myanmar



Ujumbe wa Bunge la Iran kuitembelea MyanmarMsemaji wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Nje ya Bunge la Iran amesema Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran na ujumbe wa Bunge la Iran utafanya safari nchini Myanmar katika siku zijazo. Seyyid Hussein Taqavihuseini sambamba na kuashiria jinai za kutisha na mauaji ya umati yanayofanywa dhidi ya Waislamu wa Myanmar amesema, kuendelea mauaji hayo ni jambo la kusikitisha lakini cha kusikitisha zaidi ni kukaa kimya taasisi za kimataifa na jumuiya za kutetea haki za biandamu ambazo hazijaonyesha radiamali yoyote kuhusiana na jinai hizo.

Rais Zuma na Motlanthe wakosoana hadharani



Rais Zuma na Motlanthe wakosoana hadharaniRais Jacob Zuma wa Afrika Kusini na makamu wake Kgalema Motlanthe wamekosoana hadharani mbele ya wanahabari jambo lililoonyesha kuwepo vita vya kung'ang'ania madaraka ndani ya chama tawala nchini humo ANC. Mapema Makamu wa Rais wa Afrika Kusini alikuwa amesema kwamba nchi iko katika hali ngumu na kwamba uchumi umesimama. Baadaye Rais

Wanamgambo wa ash Shabab wawaonya Waingereza



Wanamgambo wa ash Shabab wawaonya WaingerezaKundi la wanamgambo wa ash Shabab nchini Somalia limetishia kufanya mashambulizi dhidi ya Uingereza.
Shirika la Habari la Ufaransa limenukuu taarifa ya kundi hilo ikisema kuwa: Uingereza lazima ilipe gharama kubwa za vita vyake dhidi ya Uislamu na kitendo chake cha kumrejesha Sheikh Abu Hamza wa Uingereza nchini Marekani.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ash Shabab imetishia kufanya mashambulizi makali zaidi dhidi ya London kuliko yale ya tarehe 7 na 21 Julai 2005.
Itakumbukwa kuwa, miripuko ya mabomu ya tarehe 7 Julai 2005 ilipelekea watu 52 kuuwa mjini London Uingereza. Wiki mbili baadaye miripuko mingine minne ya mabomu ilitokea kwenye mfumo wa usafiri wa umma mjini humo.
Somalia haina serikali kuu tangu mwaka 1991 na tangu wakati huo hadi hivi sasa makundi mbalimbali ya watu wenye silaha yamekuwa yakijitokeza nchini humo kwa ajili ya kujidhaminia mambo tofauti.

Ghasia zaendelea Kisumu kwa siku ya pili



Ghasia zaendelea Kisumu kwa siku ya pili
Ghasia na machafuko yameendelea kwa siku ya pili mfululizo katika mji wa maghribi mwa Kenya wa Kisumu baada ya mauaji ya jana ya mwanasiasa wa chama cha ODM.
Polisi ya Kenya imetumia gesi ya kutoa machozi kujaribu kuwatawanya mamia ya vijana waliokuwa wakiandamana kupinga mauaji ya Shem Onyango Kwega, aliyetarajiwa kugombea kiti cha ubunge kwa tiketi ya chama cha Waziri Mkuu Raila Odinga ODM katika uchaguzi uliopangwa kufanyika mwakani.

Monday, October 29, 2012

Usafiri wa Treni Dar es Salaam Wanza Rasmi Leo, Dk. Mwakyembe Azindua


 
Baadhi ya abiria wakiingia kwenye treni wakati wa uzinduzi rasmi wa usafiri wa treni kutoka Ubungo mpaka Stesheni jijini Dar es salaam.
 
Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe (katikati) akiwasili kupanda treni kituo cha tazara kuelekea mjini kufanya uzinduzi
 
Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe ndani ya treni
…………………………………………….
USAFIRI wa kutumia treni jijini Dar es Salaam kutokea eneo la Ubungo Maziwa kuelekea katikati ya Jiji la Dar es Salaam (Stesheni ya Treni) umeanza leo. Treni ya kwanza imeondoka Ubungo majira ya saa 12:00 asubuhi kuelekea katikati ya jiji, ambapo kwa mujibu wa maofisa wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) imetumia wastani wa dakika 30 kufika katikati ya jiji.
Treni ilioanza kazi leo iliyokuwa na injini mbili (vichwa vya traini) moja ikiwa imefungwa nyuma na nyingine mbele huku ikiwa na mabehewa sita, yaani matano ya abiria wa kawaida (watu wazima)

SERIKALI YATOA UBANI KWA WAFIWA WA MAREHEMU KOPLO SAID ABDULRAHMAN JUMA


 
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja  Mhe,Abdalla
Mwinyi Khamis,(kulia) akikabidhi fedha kwa ajili ya Ubani kwa Niaba ya
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
 Shein,nyumbani kwa wafiwa wa Marehemu Koplo Said Abdulrahman Juma
Hassan wa Jeshi la Polisi, Nyerere Mjini Zanzibar  leo ,kwa niaba ya
wanafamilia  wa marehemu  Baba Mdogo Juma Omar Salum,(wa pili
kushoto),akipokea ubani, Mkuu wa Jeshi la  Polisi Tanzania  IGP Said
Ali Mwema,(wa pili kulia) na Baba Mzani wa Marehemu,Abdulrahman Juma
Hassan,(kushoto) . [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja  Mhe,Abdalla
Mwinyi Khamis,(katikati) akitoa nasaha zake kwa wanafamilia wa
Marehemu Koplo Said Abdulrahman Juma  Hassan wa Jeshi la POLISI
,alipofika  kukabidhi fedha kwa ajili ya Ubani kwa Niaba ya Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein,nyumbani kwa wafiwa  Nyerere Mjini Zanzibar  leo ,wengine
kushoto  Mkuu wa Jeshi la  Polisi Tanzania  IGP Said Ali Mwema,
(kushoto) na kutoka kulia Kamishna wa Polisi Zanzibar MUssa Ali Mussa
na Afisa  Tawala Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahamoud,),hafla
hiyo ilifanyika leo. [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.

WAFANYAKAZI WATAKA TAZARA IGAWANYWE KILA NCHI IJIENDESHE YENYEWE


 
CHAMA cha Wafanyakazi wa Reli nchini (TRAWU), kimetishia kugoma iwapo Serikali haitatekeleza madai yao ya kuligawa Shirika la Reli la Tanzani na Zambia (TAZARA), ili kila nchi ijiendeshe yenyewe.
 Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa chama hicho, Erasto Kihwele, alisema uwamuzi huo umefikiwa hivi karibuni kwenye mkutano  wa kujadili kwa kina hali ya uendeshaji wa shughuli za Reli nchini, uliyofanyika mjini Morogoro.
 
Alisema wamefikia hatua hiyo kutokana uendeshaji shirika hilo kuwa mgumu sana kutokana   na maamuzi mengi kuingiliana katika utekelezaji wake.

UVUNJIFU WA HAKI ZA BINADAMU, MATESO NA MAUWAJI YA WASIO NA HATIA ZANZIBAR, CUF YATOA TAMKO KALI


MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI TAREHE 29/10/2012
SERIKALI INAUKUZA MGOGORO ULIOPO BADALA YA KUUDHIBITI

Ndugu Waandishi wa Habari,
Kwanza napenda kuchukua fursa hii kutoa shukrani zangu za dhati kwenu kwa kukubali wito wa kuja kutusikiliza. Sisi Chama cha Wananchi, CUF, tunatambua na tunathamini mchango wenu mkubwa na jitihada zenu nyingi, katika kusaidia kuhamasisha hali ya amani na utulivu ndani ya nchi yetu. Ni katika kuendeleza hali ya amani na utulivu ndani ya Nchi, suala lililopelekea kukuiteni leo hapa na kukuelezeni kile ambacho sisi tunakiona kuhusiana na hali tete inayoendelea hapa Zanzibar, na Tanzania kwa ujumla.

Ndugu Waandishi,
Naamini mnatambua kuwa Msingi mmoja, Mkuu wa Chama cha

KIJANA HAMAD ALI KAIMU ALIYEUWAWA MIKONONI MWA VYOMBO VYA DOLA


231

Baba wa marehemu anasimulia mtoto wake alikamatwa siku ya sikukuu mosi akipeleka ng’ombe wake malishoni na akiwa na pesa shilingi elfu 80 ambazo shilingi elfu 30 alichangiwa na baba yake. Pesa hizo alikusudia kwenda kununua godoro baada ya kumaliza kufunga ng’ombe wake. Baba mtu alipomuona mtoto wake nje ameshikwa na polisi wasiopungua 20 alikwenda kusikiliza kumezidi nini? La haula baba mtu alipigwa na kutakiwa aondoke mara moja. Baba mtu baada ya kushuhudia mtoto wake akipata kipigo hakua na cha kufanya aliondoka na kumwacha mtoto wake mikononi mwa askari hao. Baada ya kufika jioni na kuona mtoto wake hajarejea, baba mtu alikwenda kituo cha polisi Mwanakwerekwe kumtafuta mtot wake lakini alimkosa ndipo alipokwenda kito kikuu cha polisi Madema na kumkosa pia. Ndipo baadae akapokea simu kuwa mtoto wake ameshafariki na yupo chumba cha kuhifadhia maiti hospitali ya Mnazi mmoja na kumkuta akiwa katika hali kama hiyo

Kiongozi wa Al-Qaeda awashambulia Obama na Mursi



Kiongozi wa Al-Qaeda awashambulia Obama na Mursi
Kiongozi wa mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeda Ayman Al-Zawahiri amewashambulia vikali Marais Barack Obama wa Marekani na Mohammad Mursi wa Misri akiwaita waongo na wasaliti wakubwa. Kwenye kanda mpya ya video, kiongozi huyo wa Al-Qaeda amemtaka Rais Obama kukiri kwamba Washington imeshindwa katika vita vya Iraq na Afghanistan badala ya kuwahadaa Wamarekani kwamba nchi hiyo imefanikiwa katika maeneo hayo. Amesema Marekani ililazimika kuondoka Iraq kwa madhila na pia haina budi kuondoka Afghanistan kichwa chini. Akimhutubu Rais wa Misri, al-Zawahiri ambaye ni mzaliwa wa Misri amesema Dkt. Mursi ni msaliti ambaye baada ya kuingia madarakani alitupilia mbali takwa la wanamapinduzi la kuundwa dola la Kiislamu. Ametoa wito kwa Wamisri kuendelea na harakati za mapinduzi ili kuwang’oa vibaraka wa Marekani.

Utawala wa Saudia waharibu athari za Kiislamu Madina



Utawala wa Saudia waharibu athari za Kiislamu MadinaUtawala wa Saudi Arabia unaendelea kuharibu turathi za Kiislamu zilizokuwa zimebakia katika mji wa kihistoaria wa Madina.
Kwa mujibu wa gazeti la Uingereza la Independent, katika miezi ya hivi karibuni Wasaudia walibomoa athari nyingi za Kiislamu zilizokuwa zimebakia katika maeneo tofauti ya mji mtakatifu wa Madina kwa kisingizio cha ukarabati wa nyumba zilizochakaa katika mji huo. Katika ripoti hiyo imeelezwa kuwa, utawala huo wa Aal Saud umebomoa misikiti mitatu inayohesabika kuwa ya kihistoria katika

Wanajeshi 11 wa Somalia wauawa na Al-Shabab



Wanajeshi 11 wa Somalia wauawa na Al-Shabab
Kwa akali wanajeshi 11 wa serikali ya Somalia wameuawa katika mapigano baina yao na kundi la wanamgambo wa Al-Shabab. Mapigano hayo yalizuka katika mji wa Afgoye wa kusini mashariki mwa nchi hiyo  na kwamba, kanali wa ngazi za juu wa jeshi ni miongoni mwa waliouawa katika mapigano hayo.

Jonathan: Serikali ya Nigeria itapambana vikali ugaidi


Jonathan: Serikali  ya Nigeria itapambana vikali ugaidi
Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria amesema kuwa, serikali yake itapambana vikali na mashambulio ya kigaidi na vitendo vya utumiaji mabavu ambavyo vinahatarisha usalama wa nchi hiyo. Rais wa Nigeria amesema hayo katika radiamali yake kwa mlipuko wa jana katika mji wa Kaduna wa kaskazini mwa nchi hiyo ambao ulililenga kanisa moja mjini humo na kuuawa kwa uchache watu wanane. Amesema, serikali itaendelea kupambana na vitendo

Waislamu wa Myanmar wazidi kuteseka


Waislamu wa Myanmar wazidi kutesekaRipoti mbalimbali kutoka Myanmar zinasema kuwa maafa makubwa yanatokea katika kambi ya wakimbizi wa Kiislamu katika jimbo la Rakhine. Kanali ya televisheni ya Press imeripoti kuwa watu karibu 20 wakiwemo watoto wadogo wamefariki dunia katika kambi hiyo ya Waislamu wa jamii ya Rohingya huko Myanmar kutokana na ukosefu wa dawa na chakula. Ripoti hiyo inasema

Iran yazitaka asasi za kimataifa zizuie jinai za Israel



Iran yazitaka asasi za kimataifa zizuie jinai za IsraelMsemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amezitaka asasi za haki za binadamu kuzuia  kuendelea jinai za utawala haramu wa Israel dhidi ya taifa madhulumu la Palestina. Ramin Mehmanparast amelaani mashambulio ya kigaidi ya hivi karibuni ya Israel huko Gaza na kusisitiza kwamba, jinai hizo zinazidi kubainisha utambulisho wa utawala huo ghasibu. Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amezitaka taasisi za

Daktari anayewatibu waliobakwa Kongo alengwa


Daktari anayewatibu waliobakwa Kongo alengwa
Polisi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamempeleka mahala salama daktari anayewatibu wanawake waliobakwa mashariki mwa nchi hiyo baada watu wenye silaha kufanya jaribio la kumuua.
Duru sinasema Daktari Denis Mukwege aliondolewa haraka kutoka mji wa Bukavu siku ya Jumamosi ambako amekuwa akiwatibu maelfu ya wanawake na watoto waliobakwa. Alkhamisi usiku watu watano wenye silaha

Mapigano makali yazuka tena mashariki Kongo DRC



Mapigano makali yazuka tena mashariki Kongo DRC
Mapigano makali yameripotiwa kutokea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kati ya vikosi vya serikali na waasi wa M23. Maafisa wa jeshi la Kongo wameripotiwa na duru za habari wakisema kuwa, mapigano hayo yametokea kati ya pande mbili katika jimbo la Kivu Kaskazini. Hata hivyo hakuna taarifa zaidi zilizoripotiwa kuhusiana na matokeo ya mapigano

Sunday, October 28, 2012

Mpalestina auawa shahidi katika hujuma ya Israel



Mpalestina auawa shahidi katika hujuma ya IsraelMpalestina ameuawa shahidi na mwingine kujeruhiwa katika hujuma ya angani ya utawala haramu wa Israel huko Gaza.
Duru zinasema kuwa,  alfajiri ya leo, Israel imetumia ndege ya kivita isiyo na rubani (drone) kuvurumisha makombora katika mji wa Rafah.
Utawala wa kibaguzi wa Israel umeshadidisha na kupanua mashambulizi yake dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.  Ehud Barak Waziri wa Vita wa Israel amesema kuwa, wataendelea kufanya mashambulizi huko Gaza. Wapalestina milioni 1.7 huko Gaza wanishi katika mzingiro wa Israel tokea mwaka 2007 ambapo wananyimwa haki za kimsingi kama vile madawa, chakula, elimu n.k.

Ban aonya mauaji mapya ya Waislamu wa Myanmar


Ban aonya mauaji mapya ya Waislamu wa Myanmar
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameelezea wasiwasi wake kutokana na kuanza tena wimbi jipya la mauaji ya Waislamu wa Myanmar na mapigano mengine ya kikabila nchini humo na kuitaka serikali ya nchi hiyo kukomesha haraka iwezekanavyo machafuko hayo. Ban Ki moon ametoa taarifa hiyo baada ya kuuawa kwa akali watu 56 katika jimbo la Rakhine na kuongeza kuwa, wimbi la machafuko lililotokea hivi karibuni katika

'Kikwete hana ubavu wa kupambana na rushwa Tanzania'



'Kikwete hana ubavu wa kupambana na rushwa Tanzania' Katibu Mkuu wa chama cha upinzani cha CHADEMA nchini Tanzania, Dkt. Willibrod Slaa amemkosoa Rais Jakaya Kikwete akidai kuwa hana ubavu wa kupambana na rushwa kwa kuwa chama chake cha CCM kiliingia madarakani kwa rushwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005. Dkt. Slaa amesema rushwa inazidi kukua siku hadi siku nchini Tanzania bila ya ikulu kuchukua hatua yoyote. Katibu Mkuu wa CHADEMA amesema Rais Kikwete anatania kuhusu tatizo la rushwa kwa kulizungumza tu majukwaani, huku akiwalinda washirika wake.

Rais Kikwete ashiriki mazishi ya Luteni Kanali (Mstaafu) Mussa Mrisho Mtengwa


 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiifariji familia ya Marehemu Luteni Kanali Mussa Mrisho Mtengwa nyumbani kwa marehemu kijijini  Kiwangwa,wilayani Bagamoyo leo jioni wakati Rais Kikwete alipokwenda kushiriki mazishi ya Marehemu.
 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka udongo katika kaburi la marehemu Luteni Kanali Mussa Mrisho Mtengwa wakati wa mazishi yaliyofanyika nyumbani kwa marehemu kijiji cha Kiwangwa wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani leo jioni.
Enzi za Uhai wake Marehemu Luteni Kanali Mtengwa aliwahi kuwa mpambe wa Rais wa awamu ya Pili Ali Hassan Mwinyi,kuanzia mwaka 1995 hadi mwaka 1995.Marehemu aliwahi pia kufanya kazi katika Wizara ya Sheria na kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya jeshi.
Marehemu alifariki juzi tarehe 25 Oktoba nyumbani kwake Kijitonyama jijini Dar es Salaam baada ya kuugua kwa muda na ameacha mjane watoto wanne na wajukuu watatu(picha na Freddy Maro).

Saturday, October 27, 2012

DR SHEIN, ENZI ZA WIZARA NDOGO YA KISONGE ZIMEKWISHA, CHONDE CHONDE!



Dr Shein
Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi, Dr Ali Moh’d Shein
Maskani za CCM zinafahamika na kila mwenye kufuatilia siasa za Zanzibar. Ni genge la watu ambao wengi wao hawakupata bahati ya kwenda skuli ambao walikusanywa na utawala wa Dr. Salmin Amour na kujengewa majengo kwa ajili ya kupotezea muda na kushiriki shughuli za siasa za chama hicho. Maskani kuu ni ile inayoitwa KISONGE iliyop
o katika eneo la Michenzani round about. Fikra za kimaskani zote na malengo yake ni sawa na maskani hii kaka ya KISONGE. Lengo ilikuwa ni kuwatumia wanamaskani kama hazina ya kuzalishia nguvu kazi inayohitajika katika hujuma mbali mbali zinazokilenga chama cha CUF, wafuasi wa CUF, wazanzibari wanaoipenda nchi yao, viongozi wa CUF na wazanzibari wenye asili ya Pemba. Genge hilo lilipewa maarifa, ujuzi, mbinu na uwezo wa kutosha ili kutekeleza kwa ufanisi hujuma dhidi ya walengwa. Kwanza kabisa

Friday, October 26, 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AWEKA JIWE LA MSINGI MSIKITI MPYA WA JIHAD WILAYA YA MWANGA-KILIMANJARO


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi katika Jengo la Msikiti mpya wa Jihad, baada ya kuzindua rasmi Msikiti huo uliopo katika Kijiji cha Vuchama Wilaya ya Mwanga, Mkoa wa Kilimanjaro, leo Oktoba 26, 2012 wakati wa Sikukuu ya Eid El Hajj, iliyofanyika sambamba na uzinduzi wa Mfuko wa uchangishaji fedha kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Awali, Msingi na Sekondari ya Vuchama Mosque Islamic Centre. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waumini wa Dini ya Kiislam katika Swala ya Idd El Hajj, iliyofanyika Kitaifa katika Msikiti mpya wa Jihad, uliopo katika Kijiji cha Vuchama Wilaya ya Mwanga, Mkoa wa Kilimanjaro. Ibada hiyo ilifanyika sambamba na uzinduzi wa Msikiti huo na uwekaji wa Jiwe la Msingi pamoja na uzinduzi wa Mfuko wa uchangishaji fedha kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Awali, Msingi na Sekondari ya Vuchama Mosque Islamic Centre, leo Oktoba 26, 2012. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa Swala ya Idd El Hajj, iliyofanyika Kitaifa katika Msikiti mpya wa Jihad, uliopo katika Kijiji cha Vuchama Wilaya ya Mwanga, Mkoa wa Kilimanjaro. Ibada hiyo ilifanyika sambamba na uzinduzi wa Msikiti huo na uwekaji wa Jiwe la Msingi pamoja na uzinduzi wa Mfuko wa uchangishaji fedha kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Awali, Msingi na Sekondari ya Vuchama Mosque Islamic Centre, leo Oktoba 26, 2012. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipunga mkono kuwaaga wananchi na waumini wa dini ya Kiislam, wakati akiondoka eneo hilo.

The man arrived in Makkah on foot


Subhan'Allah ,,, Ma'Sha'Allah

A 47-year-old Bosnian Muslim reach Makkah after a 3,600 miles (6000km)journey on foot from his home in Bosnia to perform pilgrimage.

Senad Hadzic, a professor of economics, started from his hometown in northern Bosnia back in December 2011.

Hadzic says.

“By this act, I am proving that everything I do is for the love of Allah ,” “For all the riches in the world, I would never stop what I am doing.”

Thursday, October 25, 2012

Wiki ya kujibari na taghuti nchini Bahrain

Wiki ya kujibari na taghuti nchini Bahrain
Wananchi wanamapinduzi wa Bahrain wamesema, sambamba na kuonyesha mshikamano wao na wananchi wenzao waliowekewa mzingiro katika mji wa al Akar wanaitangaza wiki hii kuwa ni wiki ya “Kujibari na Taghuti”. Muungano wa Vijana wa Februari 14 umeeleza kwamba katika kuendeleza harakati ya malalamiko ya wananchi wanaitangaza wiki hii kuwa ni wiki ya “Kujibari na Taghuti”. Harakati hiyo imewataka wananchi wote wa Bahrain kutumia suhula zote za kisheria ili kuuondoa mzingiro

Kura ya maoni ya katiba Zimbabwe kufanyika mwakani



Kura ya maoni ya katiba Zimbabwe kufanyika mwakani
Afisa wa ngazi za juu katika chama cha ZANU-PF nchini Zimbabwe amedokeza kwamba, kura ya maoni kuhusu katiba mpya huenda ikafanyika mwezi Januari mwaka ujao wala sio mwezi ujao kama alivyokuwa ameashiria Rais Robert Mugabe hivi majuzi. Paul Mangwana, mwenyekiti wa kamati ya bunge inayoshughulikia mchakato wa kupatikana katiba mpya amesema kuwa,

Tanzania: Ramani mpya hailengi kuichokoza Malawi



Tanzania: Ramani mpya hailengi kuichokoza Malawi
Balozi wa Tanzania nchini Malawi amesema ramani mpya ya nchi yake hailengi kupanua utata ulioko wa mpaka na nchi jirani ya Malawi. Patrick Tsere ameongeza kuwa ramani ya Tanzania  haijabadilika katika maeneo ya mipaka na amesisitiza kwamba mabadiliko ya ramani ni ya ndani kufuatia kubuniwa wilaya mpya. Mwezi uliopita Malawi ilijiondoa kwenye meza ya mazungumzo na Tanzania baada ya serikali ya Dar es Salaam kutangaza kwamba nchi ina ramani mpya. Lilongwe ilidai kwamba ramani hiyo

15 wauawa katika mashambulio ya kigaidi Iraq



15 wauawa katika mashambulio ya kigaidi Iraq
Watu wasiopungua 15 wameuawa nchini Iraq na makumi ya wengine kujeruhiwa katika wimbi jipya la mashambulio ya kigaidi yaliyoikumba nchi hiyo.  Maeneo yaliyokumbwa na mashambulio hayo ya kigaidi ni al-Mushadah kaskazini mwa Baghdad na Fallujah katika mkoa wa al-Anbar. Taarifa zaidi zinasema kuwa, mashambulio hayo ya kigaidi yaliyotokea katika maeneo ya kaskazini na katikati mwa Iraq yamezusha wasi wasi mkubwa baina ya wananchi. Mashambulio hayo yametokea katika hali ambayo kwa majumaa kadhaa sasa Iraq imeshuhudia hali ya utulivu wa kiwango fulani.  Vyombo vya usalama vya Iraq vimeimarisha usalama katika maeneo yaliyotokea mashambulio hayo.

Viongozi wa Uamsho waongezewa mashtaka, wakosa dhamana warudishwa rumande



Kiongozi wa Jumuiya ya UAMSHO Sheikh Farid Hadi Ahmed kushoto akiwa na wenzake sita walioletwa Mahakama kuu Zanzibar Vuga wakiwa hawana ndevu na kufunguliwa mashtaka manne mapya mahakamani hapo yakiwemo kuharibu mali za watu zenye thamani ya Shl.Milioni 50 na kufanya vurugu za makusudi zakuhatarisha amani katika nchi


Baadhi ya Askari wa kutuliza fujo wakiwa Mahakama kuu Zanzibar Vuga kwa lengo la kutuliza amani Mahakamani hapo



Baadhi ya Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO wakiwa wanatoka katika Mahakama Kuu ya Zanzibar Vuga baada ya kufunguliwa mashtaka manne mapya..

Mawakili wa Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO Abdallah Juma kushoto na Salim Tawfik wakizungumza na waandishi wa habari kuhusu kujitoa kwao siku ya leo katika kesi hiyo kutokana na usmbufu wanaofanyiwa wateja wao wa kuhawangaishwa na kukosa kupelekwa Mahakama ya Kwerekwe kwa muda muafa.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar

Tuesday, October 23, 2012

MAALIM SEIF ASEMA KUTOKUWEPO KWA MIKAKATI IMARA YAKUENDESHA NCHI NDIO CHANZO CHA MIGOGORO.

Katibu mkuu wa chama cha wananchi cuf maalim seif sharif hamah Amedai kuwa chanzo kikuu cha migogoro ya kijamii ikiwemo ya ardhi na mizozo ya kidini inatokana na kutokuwepo kwa mikakati imara ya kuendesha nchi, na kwamba viongozi wanapaswa kujifunza kutokana na migogoro hiyo, ili kuweka mikakati imara ya kuendesha nchi kwa uhakika.
Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar ametoa kauli hiyo katika viwanja vya Buguruni jijini Dar es Salaam alipokuwa akiwahutubia wafuasi na wapenzi wa chama hicho kwenye mkutano maalum wa hadhara uliolenga kuwakaribisha wanachama wapya na kuwapokea wanachama walioamua kurejea CUF baada ya kukihama na kuhamia vyama vyengine.
Aidha Maalim Seif amesema kuwa Tanzania imekuwa ikipita katika kipindi kigumu cha migogoro na uvunjifu wa amani, mambo ambayo yanapaswa kupigwa vita ili kurejesha hali ya amani na kuvumiliana.
Kiongozi huyo ameongeza kuwa chama chake kitaendelea kutetea na kutekeleza sera yake ya kuwaunganisha watanzania popote walipo bila ya ubaguzi wa aina yoyote.
Amesema operesheni mchakamchaka hadi mwaka 2015 iliyozinduliwa na chama hicho hivi karibuni imekuwa ni sehemu ya utekelezaji wa sera hiyo, na kwamba tayari imeanza kuleta mafanikio katika mikoa iliyoanza kutekelezwa ukiwemo mkoa wa Arusha.
Katika mkutano huo Maalim Seif aliwapokea na kuwapa kadi za chama hicho wanachama kadhaa walioamua kurejea chama hicho wakitokea chama cha ADC wakiongozwa na aliyekuwa

Mwanamke mweusi achomwa moto Marekani



Mwanamke mweusi achomwa moto Marekani
Mwanamke wa Kimarekani mwenye asili ya Afrika ameshambuliwa kwa kupigwa na kisha kuchomwa moto na kundi la vijana wenye fikra za kibaguzi katika jimbo la Louisiana nchini Marekani.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 20 alishambuliwa na kuchomwa moto vibaya kifuani na miguuni na Wamarekani weupe akiwa anatembea ndani ya bustani ya Winnsboro huko Louisiana. Taarifa zinasema kuwa, watu

4 wauawa Ethiopia katika maandamano ya Waislamu



4 wauawa Ethiopia katika maandamano ya Waislamu
Watu wanne wameripotiwa kuuawa nchini Ethiopia akiwemo polisi mmoja baada ya Waislamu waliokuwa wakiandamana kuvamia korokoro moja wanakoshikiliwa Waislamu wenzao ambao wanatuhumiwa kuzusha ghasia.
Mauaji hayo ya Waislamu nchini Ethiopia yametokea baada ya kufanyika uchaguzi wa jumuiya ya Waislamu katika mji wa Gerba

Fadhila Za Siku Ya 'Arafah Na Yawmun-Nahr (Siku Ya Kuchinja)


‘Arafah ni jabali ambalo alisimama Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwahutubia Maswahaba alipotekeleza Hijja ya kuaga. Na hapo ndipo wanaposimama Mahujaji kutimiza kilele cha ‘Ibaadah hii ya fardhi. Kusimama hapo ndio nguzo mojawapo kuu ya Hijjah bila ya kuweko hapo mwenye kuhiji atakuwa hakutimiza hijja yake kutokana na dalili  ifuatayo:

عن عبد الرحمن بن يعمر قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم:  ((الْحَجُّ عَرَفَة ، مَنْ جَاءَ قَبْلَ طُلُوعِ الْفَجْرِ مِنْ لَيْلَةِ جَمْعٍ فَقَدْ أَدْرَكَ الْحَجّ))  صحيح الجامع   

Kutoka kwa ‘Abdur-Rahmaan bin Ya’mur ambaye amesema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Al-Hajj ni ‘Arafah, atakayekuja kabla kutoka Alfajiri usiku wa kujumuika atakuwa ameipata Hajj)) [Swahiyh Al-Jaami’].

Monday, October 22, 2012

Viongozi wa Uamsho wafikishwa mahakamani Mwanakwerekwe, Wakosa dhamana warudishwa rumande


 Gari la Polisi la pili ambalo liliwachukuwa Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO ambao walishitakiwa kwa makosa ya kufanya fujo na uchochezi likiwa linasindikizwa na magari ya Polisi kuja Mahakama ya Wilaya ya Mwanakwerekwe.
 Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wakiwa wanaimarisha usalama katika eneo la Mahakama ya Wilaya Mwanakwerekwe ambapo Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO walipelekwa kwenda kusomewa mashitaka yao

 Mmoja kati ya Viongozi wa UAMSHO Shekh Azan Khalid Hamdan (43) akishuka kwenye gari la Polisi kuelekea Mahakamani Mwanakwerekwe kwenda kusomewa mashtaka yao.
  Kiongozi wa Jumuiya ya UAMSHO Shekh Farid Hadi Ahmed akishuka kwenye gari la Polisi kuelekea Mahakama ya Mwanakwerekwe kwenda kusomewa mashtaka yao yanayomkabili ikiwemo kusababisha fujo na uchochezi
 Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wakiwa wanaimarisha usalama katika eneo la Mahakama ya Wilaya Mwanakwerekwe ambapo Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO walipelekwa kushitakiwa


 Baadhi ya Wananchi walioenda Mahakamani hapo kwenda kushuhudia kesi inayowakabili Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO ambao walikosa dhamana na kurudishwa Rumande.