Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, October 25, 2012

Tanzania: Ramani mpya hailengi kuichokoza Malawi



Tanzania: Ramani mpya hailengi kuichokoza Malawi
Balozi wa Tanzania nchini Malawi amesema ramani mpya ya nchi yake hailengi kupanua utata ulioko wa mpaka na nchi jirani ya Malawi. Patrick Tsere ameongeza kuwa ramani ya Tanzania  haijabadilika katika maeneo ya mipaka na amesisitiza kwamba mabadiliko ya ramani ni ya ndani kufuatia kubuniwa wilaya mpya. Mwezi uliopita Malawi ilijiondoa kwenye meza ya mazungumzo na Tanzania baada ya serikali ya Dar es Salaam kutangaza kwamba nchi ina ramani mpya. Lilongwe ilidai kwamba ramani hiyo
imeathiri mpaka wa Ziwa Nyasa unaozozaniwa na pande mbili hizo. Malawi tayari imeiburuza Tanzania mbele ya vyombo vya sheria vya Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa kufuatia mvutano huo.
Na: Salim Swaleh

No comments:

Post a Comment