Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, October 28, 2012

'Kikwete hana ubavu wa kupambana na rushwa Tanzania'



'Kikwete hana ubavu wa kupambana na rushwa Tanzania' Katibu Mkuu wa chama cha upinzani cha CHADEMA nchini Tanzania, Dkt. Willibrod Slaa amemkosoa Rais Jakaya Kikwete akidai kuwa hana ubavu wa kupambana na rushwa kwa kuwa chama chake cha CCM kiliingia madarakani kwa rushwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005. Dkt. Slaa amesema rushwa inazidi kukua siku hadi siku nchini Tanzania bila ya ikulu kuchukua hatua yoyote. Katibu Mkuu wa CHADEMA amesema Rais Kikwete anatania kuhusu tatizo la rushwa kwa kulizungumza tu majukwaani, huku akiwalinda washirika wake.
Dkt. Slaa amezungumzia vitendo vya rushwa vilivyojitokeza katika uchaguzi wa viongozi wa CCM ni kielelezo tosha kwamba, chama hicho hakina uwezo tena wa kupambana na rushwa.

No comments:

Post a Comment