Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, October 21, 2012

Zimbabwe yajadili rasimu ya katiba mpya



Zimbabwe yajadili rasimu ya katiba mpya
Serikali ya Zimbabwe imeketi kwa shabaha ya kuchunguza rasimu ya katiba mpya ya nchi hiyo. Taarifa zinasema kuwa, kupitiwa rasimu hiyo ya katiba kunahesabiwa kuwa ni hatua muhimu yenye lengo la kumaliza hitilafu kati ya Rais Robert Mugabe ambaye pia ni kiongozi wa ZANU PF na Morgan Tsvangirai Waziri Mkuu ambaye pia ni kiongozi wa chama cha MDC. Vyama hivyo viwili viliamua kuunda serikali ya umoja wa kitaifa, baada ya kuibuka machafuko yaliyosababishwa na matokeo ya uchaguzi wa rais wa mwaka 2008. Taarifa zinasema kuwa uchaguzi ujao umepangwa kufanyika mwezi Machi 2013, huku Rais Mugabe mwenye umri wa miaka 88 akiwania kutetea kiti cha urais. Hii katika hali ambayo, wataalamu wa kiuchumi wanaeleza kuwa, hitilafu za kisiasa ni moja ya sababu kuu iliyopelekea kuongezeka umasikini, ufukara na hali mbaya ya kimaisha na kiafya kwa wananchi wa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment