Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 8, 2012

Metito aonya makundi yanayozusha fujo Kenya


Metito aonya makundi yanayozusha fujo Kenya
Waziri wa Usalama wa Taifa nchini Kenya ameyaonya makundi yanayozusha fujo nchini humo kwamba yatakabiliwa na mkono mrefu wa sheria. Katoo Ole Metito amesema makundi kama MRC na mengine ambayo yametishia kuvuruga uchaguzi mkuu ujao yatakiona cha moto iwapo yataendelea kutoa matamshi ya kijuba kama hayo. Kiongozi huyo ambaye aliteuliwa kuwa Waziri majuma kadhaa yaliyopita ameahidi kutembea kila kona ya nchi ili kuhakikisha kwamba amani na utulivu vinatawala kabla, wakati na baada ya uchaguzi mkuu ujao. Hii ni katika hali ambayo, Waziri wa Uvuvi  wa Kenya Amason Kingi alinusurika kifo siku chache zilizopita baada ya mkutano wake kuvamiwa na vijana wanaodaiwa kuwa wanachama wa MRC. Msemaji wa MRC Rashid Mraja hata hivyo amekanusha madai hayo na kusema hizo ni njama za kuzima kilio cha kundi lake cha kutafuta haki za Wapwani ambao wamenyanyaswa kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment