Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, October 21, 2012

Watu 8 wauawa katika mripuko mjini Beirut, Lebanon



Watu 8 wauawa katika mripuko mjini Beirut, Lebanon
Bomu kubwa lililokuwa limetegwa kwenye gari limeripuka leo katika mtaa wa Ashrafia huko katikati mwa Beirut mji mkuu wa Lebanon na kuua watu wanane na kuwajeruhi wengine 78. Bado haijafahamika wazi iwapo mripuko huo ulikuwa umekusudiwa kumlenga shakhsia yoyote wa kisiasa wa huko Lebanon au la. Mripuko huo mkubwa wa bomu umetokea katika mtaa ambao una ofisi ya chama cha Kikristo cha Mafalanja kinachompinga Rais Bashar Assad wa Syria. Polisi ya Lebanon imethibitisha kuuawa watu wanane  na kujeruhiwa wengine 78 katika mripuko huo wa leo. Magari na majengo kadhaa pia yameharibiwa vibaya katika mripuko huo wa bomu.

No comments:

Post a Comment