Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 22, 2012

Uganda yalitaka kundi la M23 kutoanzisha mapigano

Uganda yalitaka kundi la M23 kutoanzisha mapigano Serikali ya Uganda imelitaka kundi la M23 la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo lisianzishe tena mapigano ambayo yamewalazimisha maelfu ya wakimbizi wa Kikongo kuvuka mpaka na kuingia nchini Uganda. Wito huo umetolewa na Okello Oryem, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Uganda ikiwa ni siku moja tu baada ya Harakati ya Waasi ya M23 kutishia kwamba, itaanzisha tena mashambulio dhidi ya vikosi vya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Okello Oryem amesema, Kampala inalitaka kundi hilo kuheshimu usitishaji mapigano. Kundi la M23 lilisitisha mapigano Agosti mwaka huu baada ya kukutana na Rais Yoweri Museveni mjini Kampala na kutakiwa kufanya mazungumzo na serikali ya Kinshasa. Hata hivyo Runninga Lugerero, mmoja wa viongozi waandamizi wa M23 alitishia mwishoni mwa juma akiwa huko Bunagana kwamba, kundi lao litaanzisha tena vita kutokana na kuwa, Rais Joseph Kabila wa Kongo hayuko tayari kufanya mazungumzo ya amani.

No comments:

Post a Comment