Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, October 3, 2012

Mudavadi: Wakenya wote walishiriki katika ghasia


Mudavadi: Wakenya wote walishiriki katika ghasia Naibu Waziri Mkuu wa Kenya Bw. Musalia Mudavadi amesema kuwa, Wakenya wanne wanaokabiliwa na mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 hawana hatia na kwamba makosa ni ya Wakenya wote. Bwana Mudavadi amesisitiza kwamba, Wakenya wote walishiriki katika ghasia hizo za uchaguzi. Amesema kama ninavyomnukuu, "Tuliuana wenyewe kwa wenyewe, wanawake walibakwa na watoto kudhulumiwa, sote tunapaswa kuwajibika, taifa zima lilihusika, hivyo kuwashtaki Wakenya wanne kwa niaba ya watu milioni 40 sio haki.” Mwisho wa kumnukuu. Mudavadi amesema, washukiwa hao, Uhuru Kenyatta, Mbunge wa Eldoret Kaskazini William Ruto, Francis Muthaura na mtangazaji Joshua Arap Sang wanapaswa kushtakiwa nchini Kenya. Ameongeza kuwa, Wakenya wote wanapaswa kukubali makosa yao yaliyopelekea kuzuka ghasia hizo. Aidha amesema, yeye alikuwa miongoni mwa watu waliohimiza kubuniwa mahakama maalumu ya kuwashtaki washukiwa wa ghasia za baada ya uchaguzi na kwamba, msimamo wake haujabadilika.

No comments:

Post a Comment