skip to main |
skip to sidebar
Iran yazitaka asasi za kimataifa zizuie jinai za Israel
Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amezitaka asasi
za haki za binadamu kuzuia kuendelea jinai za utawala haramu wa Israel
dhidi ya taifa madhulumu la Palestina. Ramin Mehmanparast amelaani
mashambulio ya kigaidi ya hivi karibuni ya Israel huko Gaza na
kusisitiza kwamba, jinai hizo zinazidi kubainisha utambulisho wa utawala
huo ghasibu. Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amezitaka
taasisi za
kimataifa hususan asasi za haki za binadamu kuchukua hatua za
lazima ambazo zitazuia kuendelea jinai za Wazayuni dhidi ya wananchi
madhulumu wa Palestina. Ramin Mehmanparast amezikosoa pia siasa za
kindumakuwili za madola ya Magharibi kuhusiana na kadhia nzima ya
Palestina na kulaani himaya na uungaji mkono wa madola hayo kwa utawala
wa Kizayuni wa Israel unaotenda jinai kila uchao huko Palestina
inayokaliwa kwa mabavu.
No comments:
Post a Comment