Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, October 28, 2012

Ban aonya mauaji mapya ya Waislamu wa Myanmar


Ban aonya mauaji mapya ya Waislamu wa Myanmar
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameelezea wasiwasi wake kutokana na kuanza tena wimbi jipya la mauaji ya Waislamu wa Myanmar na mapigano mengine ya kikabila nchini humo na kuitaka serikali ya nchi hiyo kukomesha haraka iwezekanavyo machafuko hayo. Ban Ki moon ametoa taarifa hiyo baada ya kuuawa kwa akali watu 56 katika jimbo la Rakhine na kuongeza kuwa, wimbi la machafuko lililotokea hivi karibuni katika
miji mitano ya jimbo hilo  ni lenye kuitia wasiwasi mno jamii ya kimataifa. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa, serikali ya Myanmar inapaswa kuchukua hatua za haraka zenye shabaha ya kukomesha machafuko nchini humo. Imeelezwa kuwa, mamia ya nyumba zimeteketezwa kwa moto na wahalifu wa Kibudha kwenye jimbo la Rakhine, huku maelfu ya watu wakiyakimbia makaazi yao.

No comments:

Post a Comment