Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, October 25, 2012

15 wauawa katika mashambulio ya kigaidi Iraq



15 wauawa katika mashambulio ya kigaidi Iraq
Watu wasiopungua 15 wameuawa nchini Iraq na makumi ya wengine kujeruhiwa katika wimbi jipya la mashambulio ya kigaidi yaliyoikumba nchi hiyo.  Maeneo yaliyokumbwa na mashambulio hayo ya kigaidi ni al-Mushadah kaskazini mwa Baghdad na Fallujah katika mkoa wa al-Anbar. Taarifa zaidi zinasema kuwa, mashambulio hayo ya kigaidi yaliyotokea katika maeneo ya kaskazini na katikati mwa Iraq yamezusha wasi wasi mkubwa baina ya wananchi. Mashambulio hayo yametokea katika hali ambayo kwa majumaa kadhaa sasa Iraq imeshuhudia hali ya utulivu wa kiwango fulani.  Vyombo vya usalama vya Iraq vimeimarisha usalama katika maeneo yaliyotokea mashambulio hayo.

No comments:

Post a Comment