Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 15, 2012

Wanajeshi wa Uingereza wapelekwa nchini Jordan



Wanajeshi wa Uingereza wapelekwa nchini Jordan Duru za Magharibi zimetangaza kuwa wanajeshi wa Uingereza wamepelekwa nchini Jordan ili kuendesha harakati dhidi ya Syria. Maafisa wa duru za kuaminika jana walitangaza kuwa mamia ya wanajeshi na washauri wa kijeshi wa Uingereza wametumwa huko Jordan ili kuendesha harakati dhidi ya Syria na kuidhibiti nchi hiyo. Kabla ya hapo Leon Panetta Waziri wa Ulinzi wa Marekani alitangaza kuwa wanajeshi maalumu kutoka jeshi la
nchi hiyo wametumwa nchini Jordan ili kudhibiti hali ya mambo katika mipaka ya Jordan na Syria. Wanajeshi wa Uingereza na Marekani wametumwa Jordan ili kuimarisha nafasi yao katika machafuko yanayoendelea huko Syria. Hii ni katika hali ambayo Jordan kila mwaka hupokea msaada wa kijeshi kutoka Marekani wa thamani ya dola milioni 500 huku idara za kijasusi za nchi hiyo zikishirikiana na mashirika ya Marekani.

No comments:

Post a Comment