Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 8, 2012

Mkuu wa polisi ya Baghdad auliwa na magaidi


Mkuu wa polisi ya Baghdad auliwa na magaidiDuru za kipolisi nchini Iraq zimetangaza habari ya kuuawa mkuu wa kikosi cha polisi mjini Baghdad, Iraq na watu wasiojulikana wenye silaha.
Nadhin Al-Tayyah ameuawa pamoja na watu aliokuwa nao alipokuwa safarini kuelekea uwanja wa ndege wa Al Muthanna katikati ya mji wa Baghdad.
Vilevile viongozi wa Iraq wametangaza kuwa, watu wenye silaha jana walishambulia kwa maguruneti maeneo kadhaa ya vituo vya barabarani na vya upekuzi mjini Baghdad na kumuua kamanda mmoja wa jeshi la nchi hiyo.
Magaidi wanaoungwa mkono na Marekani na baadhi ya nchi za Kiarabu kama Saudi Arabia wameshadidisha oparesheni za kigaidi nchini Iraq ili kwa njia hiyo waweze kuuonyesha ulimwengu kuwa, serikali ya Baghdad haina uwezo wa kudhamini usalama.

No comments:

Post a Comment