Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 1, 2012

Wasomali wa Eastleigh, Nairobi washambuliwa

Wasomali wa Eastleigh, Nairobi washambuliwa Mamia ya Wakenya waliokuwa na hasira wamewashambulia Wasomali katika mtaa wa Eastleigh, mjini Nairobi Kenya, ikiwa ni masaa machache tu baada ya kutokea mlipuko kwenye shule ya Jumapili ya watoto wa Kikristo, mlipuko ambao uliua mtoto mmoja na kujeruhi wengine kadhaa. Polisi ililazimika kufanya kazi ya ziada kulitawanya kundi la vijana waliokuwa na hasira ambalo lilikuwa likiwalenga Wasomali. Nyumba kadhaa za Wasomali zimeshambuliwa kwa mawe katika shambulio hilo. Wakenya hao wanawatuhumu Wasomali kuwa ndio waliohusika katika shambulio la bomu hapo jana katika kanisa moja jijini Nairobi. Wasomali hao walilazimika kukimbilia katika maduka au nyumba zao kuwakwepa vijana hao waliokuwa na hasira. Wakati huo huo, maafisa wawili wa polisi ya Kenya wameuawa katika mji wa Garissa eneo ambalo liko katika mpaka wa pamoja wa Kenya na Somalia. Mlipuko wa jana na mauaji dhidi ya maafisa wawili wa polisi yametajwa kuwa radiamali ya wanamgambo wa Ash Shabab wa Somalia baada ya jeshi la Kenya kuudhibiti mji wa Kismayu ambayo ni ngome ya wanamgambo hao.

No comments:

Post a Comment