Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, October 10, 2012

Jeshi la Nigeria lakanusha tuhuma za kuua raia


    Jeshi la Nigeria lakanusha tuhuma za kuua raia
Jeshi la Nigeria limekanusha kuwa askari wake juzi waliwaua watu 35 huko katika mji wa Maiduguri kaskazini mwa nchi hiyo. Watu walioshuhudia wameeleza kuwa askari jeshi wa Nigeria walifyatua risasi baada ya bomu kuripuka kwenye msafara wa jeshi na baadae askari jeshi hao wakaanza kuwapiga raia kabla ya kuendelea na ufyatuaji risasi. Wauguzi katika hospitali ya Umaru Shehu wamesema kuwa watu 30 waliouliwa na wanajeshi walikuwa wamevaa nguo za kiraia huku wengine watano wakiwa na sare za kijeshi. Luteni Kanali Sagir Musa ambaye ni msemaji wa kikosi cha pamoja cha oparesheni huko katika jimbo la Borno amesema kuwa hakuna tukio lolote linalohusisha kuuliwa raia hao 30 na kwamba kikosi hicho hakikutekeleza uchomaji wowote wa mali za raia kwa makusudi wala kuwatesa raia hao. Wanajeshi wa Nigeria wamekuwa wakituhumiwa mara kwa mara kuwa wanaua raia na kuchoma nyumba au maduka yao kufuatia miripuko ya mabomu inayowalenga wanajeshi hao

No comments:

Post a Comment