Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, October 31, 2012

Mugabe: Uchaguzi Mkuu utafanyika Machi mwakani



Mugabe: Uchaguzi Mkuu utafanyika Machi mwakani
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amesema kuwa lengo lake kuu ni kuendesha uchaguzi kote nchini humo ifikapo mwezi Machi mwakani kwa mujibu wa katiba mpya ya nchi hiyo. Mugabe amesema kuwa harakati zao zinapasa kusonga mbele licha ya mitazamo yao ya kisiasa kutofautiana. Mugabe ameyatamka hayo katika kikao kilichohudhuriwa pia na Morgan Tsvangirai Waziri Mkuu wa Zimbabwe na ambaye pia ni mpinzani wake mkuu wa kisiasa. Kamati ya katiba ya Zimbabwe imesaini rasimu ya mwisho ya katiba hiyo mpya na kuidhinishwa na karibu mirengo yote mikuu ya kisiasa na kiraia ya nchi hiyo, hata hivyo tarehe ya kufanyika kura ya maoni kuhusiana na katiba hiyo bado haijatangazwa. Kura ya maoni ndiyo itakayofungua njia ya kufanyika chaguzi zijazo za Rais na Bunge huko Zimbabwe.

No comments:

Post a Comment