Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 29, 2012

Kiongozi wa Al-Qaeda awashambulia Obama na Mursi



Kiongozi wa Al-Qaeda awashambulia Obama na Mursi
Kiongozi wa mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeda Ayman Al-Zawahiri amewashambulia vikali Marais Barack Obama wa Marekani na Mohammad Mursi wa Misri akiwaita waongo na wasaliti wakubwa. Kwenye kanda mpya ya video, kiongozi huyo wa Al-Qaeda amemtaka Rais Obama kukiri kwamba Washington imeshindwa katika vita vya Iraq na Afghanistan badala ya kuwahadaa Wamarekani kwamba nchi hiyo imefanikiwa katika maeneo hayo. Amesema Marekani ililazimika kuondoka Iraq kwa madhila na pia haina budi kuondoka Afghanistan kichwa chini. Akimhutubu Rais wa Misri, al-Zawahiri ambaye ni mzaliwa wa Misri amesema Dkt. Mursi ni msaliti ambaye baada ya kuingia madarakani alitupilia mbali takwa la wanamapinduzi la kuundwa dola la Kiislamu. Ametoa wito kwa Wamisri kuendelea na harakati za mapinduzi ili kuwang’oa vibaraka wa Marekani.

No comments:

Post a Comment