Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, October 3, 2012

Matamshi ya Rasmussen juu ya kuondoka mapema vikosi vya NATO Afghanistan

Matamshi ya Rasmussen juu ya kuondoka mapema vikosi vya NATO Afghanistan
Kuongezeka mashambulizi dhidi ya vikosi vya NATO nchini Afghanistan kulikopelekea kuuawa askari wengi wa jumuiya hiyo kumesababisha baadhi ya nchi zenye askari wake nchini humo zitake kuharakishwa kuondoka vikosi hivyo nchini Afghanistan kabla ya muda uliopangwa. Takwa hili limezidi kutolewa katika miezi ya hivi karibuni baada ya kushika kasi wimbi la mashambulio yanayofanywa na maafisa wa jeshi na polisi wa Afghanistan dhidi ya askari wa kigeni suala lililopelekea makumi ya askari hao kuuawa. Mashambulizi hayo ambayo yamepewa jina la ‘mashambulio ya ndani’ hadi sasa yamepelekea askari 52 wa NATO kuangamizwa. Kuhusiana na suala hilo Anders Fogh Rasmussen Katibu Mkuu wa Shirika la Kijeshi la Magharibi NATO sambamba na kukiri mashambulio hayo pamoja na kudhoofika morali wa askari wa jumuiya hiyo ameelezea uwezekano wa kuondoka mapema askari wa kigeni nchini Afghanistan. Rasmussen amesema, askari wa nchi za Magharibi wanaweza kuondoka Afghanistan mapema na kabla ya muda uliopangwa, kwani mashambulizi ya wanajeshi wa Kiafghani ambayo amesema yanahesabiwa kuwa stratejia mpya ya Taliban yamefanikiwa kudhoofisha morali wa askari wa kigeni. Pia katika kujibu suala la mashinikizo yanayotolewa ya kutaka kuondoka haraka vikosi vya jumuiya hiyo Afghanistan Katibu Mkuu wa NATO amesema, suala hilo linajadiliwa na kufuatiliwa na kwamba katika miezi mitatu ijayo uamuzi utachukuliwa. Aidha ameongeza kwamba, kuanzia sasa hadi mwaka 2014 majukumu na kuwepo askari wa NATO nchini Afghanistan kutategemea hali ya usalama wa nchi hiyo na kusisitiza kuwa, iwapo hali hiyo haitaimarika, suala hilo litapelekea kuharakishwa kuondoka vikosi hivyo nchini humo. Katibu Mkuu wa NATO vilevile ameshiria kuuawa askari zaidi ya 50 wa NATO mwaka huu katika mashambulizi yaliyofanywa na vikosi vya Kiafghani dhidi ya askari wa kigeni na kusema, suala hilo limeuwekea doa uhusiano kati ya vikosi vya NATO na askari polisi na jeshi la Afghanistan kwani mashambulizi hayo yameondoa kabisa uamunifu kati ya pande mbili. Marekani na washirika wake wametambua kwamba kuendelea kuwepo kijeshi vikosi vyao nchini Afghanistan hakuna faida nyingine kwao zaidi ya kuzidi kushambuliwa na kuuawa raia wa nchi hizo. Wakati huo huo kupungua bajeti ya askari wa Marekani walioko Afghanistan kumesababisha wapanga mipango wa Pentagon walazimike kupunguza operesheni za kijeshi za nchi hiyo hadi kufikia mwaka 2013. Taarifa zinaeleza kuwa, bajeti iliyotengwa na Marekani mwaka huu wa 2012 kwa ajili ya vita nchini Afghanistan ni karibu dola bilioni 118 lakini mwaka ujao wa 2013 bajeti hiyo itapungua na kufikia dola bilioni 89. Kwa mujibu wa mkakati mpya wa Marekani uliotangazwa mwaka jana na Rais Barack Obama wa nchi hiyo, Washington imesema kwamba inakusudia kuondoa polepole askari wake nchini Afghanistan na kuwaachia askari wa Kiafghani jukumu la kulinda usalama wa nchi hiyo. Lakini pamoja na mipango hiyo ya kubadilisha mikakati yake, inaonekana kuwa Marekani ina lengo la kuendelea kubakia nchini Afghanistan kwa sura nyingine kwa mujibu wa makubaliano ya kistratejia ya kiusalama ya nchi mbili hizo

No comments:

Post a Comment