Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, October 23, 2012

Fadhila Za Siku Ya 'Arafah Na Yawmun-Nahr (Siku Ya Kuchinja)


‘Arafah ni jabali ambalo alisimama Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwahutubia Maswahaba alipotekeleza Hijja ya kuaga. Na hapo ndipo wanaposimama Mahujaji kutimiza kilele cha ‘Ibaadah hii ya fardhi. Kusimama hapo ndio nguzo mojawapo kuu ya Hijjah bila ya kuweko hapo mwenye kuhiji atakuwa hakutimiza hijja yake kutokana na dalili  ifuatayo:

عن عبد الرحمن بن يعمر قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم:  ((الْحَجُّ عَرَفَة ، مَنْ جَاءَ قَبْلَ طُلُوعِ الْفَجْرِ مِنْ لَيْلَةِ جَمْعٍ فَقَدْ أَدْرَكَ الْحَجّ))  صحيح الجامع   

Kutoka kwa ‘Abdur-Rahmaan bin Ya’mur ambaye amesema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Al-Hajj ni ‘Arafah, atakayekuja kabla kutoka Alfajiri usiku wa kujumuika atakuwa ameipata Hajj)) [Swahiyh Al-Jaami’].


Fadhila Za Siku ya ‘Arafah:


1-Ni Siku Iliyokamilika Dini Yetu  

قال رجل من اليهود لعمر : يا أمير المؤمنين ، لو أن علينا نزلت هذه الآية : ((اليوم أكملت لكم دينكم وأتممت عليكم نعمتي ورضيت لكم الإسلام دينا)) لاتخذنا ذلك اليوم عيدا ، فقال عمر: "إني لأعلم أي يوم نزلت هذه الآية ، نزلت يوم عرفة ، في يوم جمعة"  البخاري

Kutoka kwa ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Myahudi mmoja alimwambia: “Ewe Amiri wa Waumini, lau ingeliteremka kwetu sisi Aayah hii ((Leo Nimekukamilishieni Dini yenu na Nimekutimzieni Neema Zangu kwenu na Nimekuridhieni Uislamu kuwa ni Diyn yenu)) [Al-Maaidah (5: 3] tungeliifanya ‘Iyd siku hiyo. Akasema ‘Umar: “Hakika naijua siku gani imeteremka Aayah hii. Imeteremka Siku ya ‘Arafah siku ya Ijumaa” [Al-Bukhaariy)


Na ukamilifu wa dini siku hiyo ni kwa vile Waislamu hawakupata kutekeleza Hajj kabla ya hapo ya Kiislamu. Na kukamilika dini yao ni kukamilisha nguzo za Kiislamu zote.  


2-Kufunga Swawm ni kufutiwa madhambi ya miaka miwili:

Ni fadhila kubwa kwetu kujitakasa na madhambi tunayoyachuma kila siku kwani binaadamu daima ni mkosa.


عَنْ أَبِي قَتَادَةَ رضي الله عنه أن النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ :  ((صِيَامُ يَوْمِ عَرَفَةَ أَحْتَسِبُ عَلَى اللَّهِ أَنْ يُكَفِّرَ السَّنَةَ الَّتِي قَبْلَهُ وَالسَّنَةَ الَّتِي بَعْدَهُ )) أخرجه مسلم

Imetoka kwa Abu Qataadah (Radhiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: “Swawm ya 'Arafah nataraji (kwa Allaah) kufuta madhambi ya mwaka uliopita na wa baada yake.” [Muslim]

Umuhimu huo wa kufunga na na msisitizo ni kwa wasiohiji, na walio katika Hajj wao hakuna msisitizo huo kwa dalili ifuatayo:

عن ميمونة بنت الحارث: أن الناس شكوا في صيام النبي صلى الله عليه وسلم يوم عرفة ، فأرسلت إليه بحلاب ، وهو واقف في الموقف ، فشرب منه والناس ينظرون" البخاري

Kutoka kwa Maymuunah bint Al-Haarith (Radhiya Allaahu ‘anhaa) kwamba watu walitia shaka na Swawm ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa  aalihi wa sallam) [kama alifunga] Siku ya ‘Arafah, nikampelekea maziwa, naye akiwa amesimama akayanywa na huku watu wanamtazama.”  [Al-Bukhaariy]

Hata hivyo, kuna baadhi ya Ma'ulamaa wanaona kuwa funga ya 'Arafah inawahusu na Mahujaji vilevile.


3-Ni Siku Bora Kabisa Ambayo Wataokolewa Waja Kutokana Na Moto; Wataghufuriwa Madhambi Yao



عن  جابر  رضي الله عنه  عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: ((مَا مِنْ يَوْمٍ أَفْضَلُ عِنْدَ اللَّهِ مِنْ يَوْمِ عَرَفَةَ، يَنْزِلُ اللَّهُ تَعَالَى إلَى سَمَاءِ الدُّنْيَا فَيُبَاهِي بِأَهْلِ الْأَرْضِ أَهْلَ السَّمَاءِ)) وروى ابن حبان
وفي رواية: ((إنَّ اللَّهَ يُبَاهِي بِأَهْلِ عَرَفَةَ مَلَائِكَتَهُ، فَيَقُولُ: يَا مَلَائِكَتِي، اُنْظُرُوا إلَى عِبَادِي، قَدْ أَتَوْنِي شُعْثا غُبْرا ضَاحِينَ))

Kutoka kwa Jaabir (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa  aalihi wa sallam) amesema: “Hakuna siku iliyo bora kabisa mbele ya Allaah kama siku ya ‘Arafah. Anateremka Allaah Ta’ala mbingu ya dunia (ya kwanza) kisha Anawafakhiri watu  ardhi  kwa watu wa mbingu.”


Na katika riwaaya nyingine: “Hakika Allaah Anawafakhiri watu ‘Arafah kwa Malaika Wake. Husema Husema Ee Malaika wangu, watazameni waja Wangu wamenijia wakiwa timtimu wamejaa vumbi …”

Pia,

 عن عائشة  رضي الله عنها عن النبي صلى الله عليه وسلم: ((ما من يوم أكثر من أن يعتق الله فيه عبيدا من النار من يوم عرفة ، وأنه ليدنو ، ثم يباهي بهم الملائكة فيقول : ما أراد هؤلاء ؟ اشهدوا ملائكتي أني قد غفرت لهم )) صحيح الترغيب

Kutoka kwa ‘Aaishah (Radhiya Allaahu ‘anhaa) kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): “Hakuna siku Anayoacha Allaah kwa wingi huru waja kutokana na moto kama siku ya ‘Arafah. Na huwa karibu kisha Anajigamba kwao kwa Malaika na Husema: Wametaka nini hawa? Shuhudieni Malaika wangu kwamba hakika Mimi Nimewaghufuria)) [Swahiyh At-Targhiyb]
  

عن جابر  رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم-(( ما من أيام عند الله أفضل من عشر ذي الحجة قال فقال رجل يا رسول الله هن أفضل أم عدتهن جهادا في سبيل الله قال: (( هن أفضل من عدتهن جهادا في سبيل الله وما من يوم أفضل عند الله من يوم عرفة ينزل الله تبارك وتعالى إلى السماء الدنيا فيباهي بأهل الأرض أهل السماء فيقول انظروا إلى عبادي جاءوني شعثا غبرا ضاحين جاءوا من كل فج عميق يرجون رحمتي ولم يروا عذابي فلم ير يوم أكثر عتيقا من النار من يوم عرفة))   الترغيب والترهيب - إسناده صحيح أو حسن 

Kutoka kwa Jaabir (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakuna Siku iliyo bora kabisa kama siku kumi za Dhul-Hijjah, akasema mtu: “Ee Mjumbe wa Allaah, hizo ni bora au Jihaadi katika njia ya Allaah? Akasema: “Hizo ni bora kuliko Jihaad katika njia ya Allaah, na hakuna siku bora kabisa mbele ya Allaah, kama siku ya ‘Arafah, Anateremka Allaah Tabaaraka wa Ta’ala katika mbingu ya dunia kisha Anawafakhiri watu wa ardhini kwa watu wa mbinguni kisha Anasema: Tazameni waja Wangu wamenijia timtimu wamejaa vumbi wamekuja kutoka kila pembe ya mbali wanataraji Rehma Yangu na wala hawajaona adhabu Yangu. Na wala hakuona siku inayoachwa huru shingo kutokana na moto kama siku ya ‘Arafah.” [At-Targhiyb wat-Tarhiyb – Isnaad yake Swahiyh au Hasan]
  
  
4.    Siku Ya Kutakabaliwa Du’aa

Amesema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa  aalihi wa sallam):

 ((خير الدعاء دعاء يوم عرفة، وخير ما قلت أنا والنبيون من قبلي: لا إله إلا الله وحده لا شريك له، له الملك وله الحمد وهو على كل شيء قدير)) روى الترمذي
  
“Du’aa bora kabisa ni du’aa katika siku ya 'Arafah, na yaliyo bora kabisa niliyosema mimi na Mitume kabla yangu ni: 'Laa Ilaaha Illa Allaah Wah-dahu Laa Shariyka Lahu, Lahul-Mulku Wa-Lahul-hamdu Wa Huwa 'Alaa Kulli Shay-in Qadiyr – Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allaah, Pekee Hana mshirika, ufalme wote ni Wake, na Sifa njema zote ni Zake, Naye ni Mweza wa kila kitu daima.” [At-Tirmidhiy]




6-     Siku Ambayo Allaah Ameiapia

Allaah Ameiapia siku hii ya ‘Arafah ambayo inajulikana kwa ‘Siku ya Kushuhudiwa’. Hii kutokana na kauli Yake Subhaanahu wa Ta’ala:
بِسْمِ اللّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ  ((وَالسَّمَاء ذَاتِ الْبُرُوجِ))  (( وَالْيَوْمِ الْمَوْعُودِ))   ((وَشَاهِدٍ وَمَشْهُودٍ))
((Naapa kwa mbingu yenye Buruji!))  ((Na kwa siku iliyoahidiwa!)) ((Na kwa shahidi na kinachoshuhudiwa!)) [Al-Buruuj 85: 1-3]

Imetoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa alihi wa sallam) amesema: “Siku ya kuahidiwa ni siku ya kufufuliwa. Siku ya kushuhudiwa ni siku ya ‘Arafah, na Siku ya kinachoshuhudiwa ni Siku ya Ijumaa)) [At-Tirmidhiy na imepewa daraja ya Swahiyh na Shaykh Al-Albaaniy]

7-Siku Ambayo Allaah Amechukua Fungamano (ahadi) Kutoka Kizazi Cha Aadam

Imesimuliwa kwamba Ibn ‘Abbaas (Radhiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa alihi wa sallam) amesema: “Allaah Amechukua fungamano kutoka mgongo wa Aadam katika Na’maan yaani ‘Arafah. Akalete mbele mgongo wake kizazi chake chote na akawatandaza mbele Yake.. Kisha Akawakabali kuwauliza:
 ((أَلَسْتَ بِرَبِّكُمْ قَالُواْ بَلَى شَهِدْنَا أَن تَقُولُواْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ إِنَّا كُنَّا عَنْ هَذَا غَافِلِينَ)) (( أَوْ تَقُولُواْ إِنَّمَا أَشْرَكَ آبَاؤُنَا مِن قَبْلُ وَكُنَّا ذُرِّيَّةً مِّن بَعْدِهِمْ أَفَتُهْلِكُنَا بِمَا فَعَلَ الْمُبْطِلُونَ))
((Je, Mimi si Mola wenu? Wakasema: Kwani! Tumeshuhudia. Msije mkasema Siku ya Qiyaamah sisi tulikuwa tumeghafilika na hayo)) ((Au mkasema: Hakika baba zetu ndio walioshirikisha kabla yetu, na sisi ni dhuriya zao tu baada yao. Basi Utatuangamiza kwa sababu ya waliyoyafanya wapotovu?)) [Al-A’araaf 7: 172-173] [Imesimuliwa na Ahmad na imepewa daraja ya Swahiyh na Shaykh Al-Albaaniy]


Kutokana na fadhila hizo, ndio ikawa ni siku tukufu kabisa na siku ambayo ruknu ya Hajj kuu inatimizwa na bila ya mtu kusimama ‘Arafah inakuwa hakutekeleza Hajj.

Fadhila Za Yawmun-Nahr – Siku ya Kuchinja:
Siku kuu ya ‘Iydul-Adhw-haa na ndio inajulikana pia kwa Yawmun-Nahr.

Kasema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): 

((إن أعظم الأيام عند الله يوم النحر، ثم يوم الق))  أبي داود

“Siku iliyo tukufu kabisa kwa Allaah ni siku ya kuchinja, kisha siku ya kutulia”  (yaani siku ya kukaa Mina)  [Abu Daawuud]
Sababu ya kuchinja ni kufuata Sunnah ya baba yetu Nabii ‘Ibraahiym (‘Alayhis Salaam) alipotaka kumchinja mwanawe Ismaa’iyl na Allaah Akamteremshia badala yake kafara ya mnyama.

No comments:

Post a Comment