Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, June 26, 2012

Hukmu Ya Muziki Katika Qur-aan Na Sunnah

Muziki ni haraam kutokana na dalili dhahiri tulizopewa katika Qur-aan na Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).
Baadhi wa watu katika Jamii yetu bado hawajatambua uharamu wa jambo hili, tunasikia wengi bado wanaimba taarabu au miziki mbalimbali, na mara kwa mara unapomnasihi nduguyo Muislamu kuacha maasi haya, jibu mara nyingi huwa: "Tena nyinyi mmezidi! Wapi inasema kuwa nyimbo haramu" Au wengine waliobobea katika maradhi haya hunena: "Mimi yote naweza kuacha lakini nyimbo utaniua", husema hivyo bila ya kujali amri ya makatazo ya Mola Mtukufu ambaye ni Muweza wa kuyaua masikio yake awe kiziwi na asiweze kusikia tena hizo nyimbo.
Inafika hadi Muislam hawezi kulala hadi alazwe kwa muziki, hawezi kula ila muziki uwe unapigwa, hawezi kufanya kazi za nyumbani bila muziki kufunguliwa, hawezi mtu kutembea bila kuwa na walkman au mp3 yake ikicheza, hawezi kufanya kazi akiwa kazini…hawezi kusafiri…hawezi hata kufanya mazoezi ya ndani bila kuwepo na muziki wa kumchochea na kumtia hamasa (kama wanavyoitakidi) ya lile analolifanya kwa wakati huo! ‘Alaa kulli haal, muziki umekuwa ni sehemu kiungo kikubwa cha maisha ya mwanaadam kwa wakati huu!
Hivyo tumeona kuna umuhimu mkubwa wa kuwakumbusha ndugu zetu waepukane na haramu hii ili wajiokoe na ghadabu za Mola Mtukufu, ghadhabu kali ambazo zinafika kumgeuza mtu awe nyani au nguruwe kama tutakavyosoma katika hizi dalili za wazi wazi zenye uhakika.
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

((وَمِنَ النَّاسِ مَن يَشْتَرِي لَهْوَ الْحَدِيثِ لِيُضِلَّ عَن سَبِيلِ اللَّهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَيَتَّخِذَهَا هُزُوًا أُولَئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ))

((Na miongoni mwa watu wapo wanaonunua maneno ya upuuzi, ili wawapoteze watu na njia ya Mwenyezi Mungu pasipo kujua, na wanaichukulia ni maskhara. Hao watapata adhabu ya kuwafedhehesha)) [Luqmaan: 6]

Ibn Mas'uud (Radhiya Allaahu 'anhu) amesema kuhusu Aayah hii "Naapa kwa Allaah hii inamaanisha ni kuimba" [At-Twabariy 20:127]

وعن ابن عباس قال عن آية: ((ومن الناس من يشتري لهو الحديث))، قال :الغناء وأشباهه إسناده صحيح - المحدث: الألباني

Na Ibn 'Abbaas (Radhiya Allaahu 'anhuma) pia amesema kuhusu Aayah: ((Na miongoni mwa watu wapo wanaonunua maneno ya upuuzi)) "Ni nyimbo na maneno ya yanayofanana (ya upuuzi)" [Isnaad Sahiyh kutoka kwa Shaykh Al-Albaaniy]
 
Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anamwambia Ibilisi:


((وَاسْتَفْزِزْ مَنِ اسْتَطَعْتَ مِنْهُمْ بِصَوْتِكَ وَأَجْلِبْ عَلَيْهِم بِخَيْلِكَ وَرَجِلِكَ وَشَارِكْهُمْ فِي الأَمْوَالِ وَالأَوْلادِ وَعِدْهُمْ وَمَا يَعِدُهُمُ الشَّيْطَانُ إِلاَّ غُرُورًا))

 
((Na wachochee uwawezao katika wao kwa sauti yako, na wakusanyie jeshi lako la wapandao farasi na waendao kwa miguu. Na shirikiana nao katika mali na wana, na waahidi. Na shaytwaan hawapi ahadi ila ya udanganyifu)) [Al-Israa: 64]
Hii inamaanisha ni nyimbo kama ilivyo rai ya Mujaahid katika Tafsiyr ya Ibn Kathiyr]
Vile vile Hadiyth zifuatazo zimedhihirisha uharamu wa nyimbo, ngoma na kila aina ya muziki:


عبدالله بن عمرو بن العاص عن رسول الله صلى الله عليه وسلم انه قال: ((إن الله حرم الخمر والميسر والكوبه وكل مسكر حرام ((إسناده صحيح

و في رواية أحمد قال سفيان: قلت لعلي بن بذيمة: "ما الكوبة؟" قال: "الطبل"
Kutoka kwa 'Abdullaah bin 'Amru ibnul 'Aasw kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika Allaah Ameharamisha pombe na kamari na kuubah na kila kilinacholewesha ni haram)) [Isnaad yake ni Sahiyh]
Na katika usimulizi mwingine kutoka kwa Imaam Ahmad, Sufyaan amesema: Nilimuliza 'Aliy ibn Budhaymah: "Nini Kuubah?" Akasema: "Ngoma".

 WENYE KUIMBA/KUSIKILIZA MUZIKI WATAGEUZWA KUWA NYANI
NA NGURUWE!

 
 وقال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((ليكونن من أمتي أقوام يستحلون الحر و الحرير و الخمر و المعازف، و لينزلن أقوام إلى جنب علم، يروح عليهم بسارحة لهم، يأتيهم لحاجة، فيقولون: ارجع إلينا غدا، فيبيتهم الله، ويضع العلم، ويمسخ آخرين قردة وخنازير إلى يوم القيامة ((رواه البخاري
 Na akasema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Watakuweko watu katika Ummah wangu watakaojaribu kuhalilisha zinaa, uvaaji wa hariri, pombe na muziki. Baadhi ya watu watakuwa pembeni mwa mlima na mchungaji wao atawajia jioni na kuwaomba haja [fulani]. Watasema: "Rudi kesho". Allaah Atawaangamiza usiku, Atawaangushia milima kisha Atawabadilisha waliobakia wawe nyani na nguruwe na watabakia hivyo hadi siku ya Qiyaamah))[Al-Bukhaariy]


Hadiyth hii inatuthibitishia kuwa madhambi yote hayo yako sawa sawa uharamu wake,
kama vile zinaa na pombe ilivyo haramu, basi na muziki pia haramu sawa sawa. Sasa vipi Muislamu aone kuwa muziki sio maasi makubwa ya kujiepusha nayo?
 
Imaam Abu Haniyfah amesema: "Kuimba (nyimbo, ngoma) ni katika madhambi makubwa ambayo inatakiwa Muislamu kujiepusha nayo haraka"
 
Khofu zaidi imuingie Muislamu kuwa anaweza kupata adhabu ya kugeuzwa nyani au nguruwe kwa maasi haya kama tulivyoonywa katika Hadiyth ifuatayo:


 
وقال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((ليشربن أقوام من أمتي الخمر يسمونها بغير اسمها يعزف على رؤوسهم بالمعازف والمغنيات ، يخسف الله بهم الأرض ويجعل منهم قردة وخنازير)) قال الشيخ الألباني- رحمه الله تعالى- : صحيح

 
Na kasema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Watu katika Ummah wangu watakunywa pombe wakiipa jina jengine lisilokuwa hilo, miziki itapigwa kwa ajili yao na watakuweko waimbaji wanawake. Allaah Atawadidimiza ardhini na Atawageuza wawe nyani na nguruwe)) [Ibn Maajah na Shaykh Al-Albaaniy ameipa daraja ya Sahiyh]



 GHADHABU ZA ALLAAH KUWAANGAMIZA WAFANYAO MAASI HAYA!


 
Vile vile ghadhabu za Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) ni kali mno za kuangamizwa pindi maasi haya yatakapodhihirika.


 عن عمر بن حصيل عن رسول الله صلى الله عليه وسلم انه قال: ((يكون فى امتى قذف ومسخ وخسف)): قيل يارسول الله ومتى ذلك قال: ((اذا ظهرت المعازف… )) اخرجه الترمذى وصححه العلامه الالبانى

 
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: ((Kutatokea katika Ummah huu maafa ya kuteremshiwa mawe kutoka mbinguni, kugeuzwa maumbile ya binaadamu [kugeuzwa kufanywa nyani na nguruwe] na mididimizo [ya ardhi]. Ikaulizwa: Ewe Mjumbe wa Allaah, lini yatatokea hayo? Akasema: ((Itakapodhihirika muziki … )) [At-Trimidhy na ameipa daraja ya Sahiyh Shaykh Al-Albaaniy]

 
 QUR-AAN NDIO NYIMBO YETU

 Muziki na nyimbo humjaza mtu mapenzi makubwa moyoni, zimshughulishe zaidi hadi asiwe na muda wa kusoma maneno ya Mola wake Mtukufu ambayo hiyo ndio inayopasa kuifanya iwe midomoni na moyoni mwetu daima kwa kusoma kwa sauti nzuri ya kupendeza (Tajwiyd) kama tulivyoamrishwa na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).



 SAUTI ZA NYIMBO ZIMELAANIWA DUNIANI
NA AKHERA

 قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((صوتان ملعونان فى الدنيا والاخره مزمار عند نعمه ورنه عند مصيبه)) البزار و صححه العلامه الالبانى

 Na kasema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Sauti mbili maluuni [zilizolaaniwa] duniani na Akhera; mizumari katika furaha na kuombeleza katika misiba)) [Al-Baazaar – na Shaykh Al-Albaaniy kaipa daraja ya Sahiyh]
 

 NI SUNNAH KUZIBA MASIKIO UNAPOSIKIA MUZIKI BILA YA KUTAKA

 
عن نافع أنه قال: سمع ابن عمر مزمارا، قال: فوضع أصبعيه على أذنيه، ونأى عن الطريق، وقال لي: يا نافع هل تسمع شيئا؟ قال: فقلت: لا! قال: فرفع أصبعيه من أذنيه، وقال: كنت مع النبي صلى الله عليه وسلم، فسمع مثل هذا! فصنع مثل هذا - حديث صحيح، صحيح أبي داوود وراجع السلسلة الصحيحة للألباني 
Kutoka kwa Naafi'i ambaye amesema, amesikia sauti ya muziki akaziba masikio yake kwa vidole vyake, kisha akamgeuza mnyama wake aliyempanda [arudi asiendelee kwenda sehemu hiyo iliyokuwa na muziki] akasema: "Ewe Naafi'i, umesikia kitu?" Akasema, nikajibu: "Hapana". Akaondosha vidole vyake masikioni mwake akasema: "[siku moja] Nilikuwa na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliposikia kama hivi [muziki] akafanya kama hivi [nilivyofanya mimi yaani kuziba masikio yake asisikie sauti ya mizumari] [Hadityh Swahiyh ya Abu Daawuud  na   Ikiwa katika Silsilatus-Swahiyha ya Shaykh Al-Albaaniy]

 

 
و قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((لا تصحب الملائكة رفقة فيها كلب ولا جرس)) مسلم
 
Na kasema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Malaika hawafuatani na watu wenye mbwa na walio na kengele)) [Muslim]
 
Tanbihi: Ikiwa kengele tu inawakimbiza Malaika, seuze nyimbo, ngoma, mizumari na aina zote za muziki ambazo zinaamsha vishawishi na kuchochea hisia za binaadamu!

 MWENYE KUMPA MWENZIWE TAARIFA AU KUMPELEKA KWENYE MUZIKI ATABEBA DHAMBI ZAKE
NA DHAMBI ZA MWENZIWE!

 Mara nyingi Waislamu wenye kufanya maasi haya wanasabisha wenzao kutumbukia pia katika maasi haya; kuna wanaoalika watu katika shughuli zenye maasi hayo (parties) zenye mchanganyiko wa wanawake na wanaume, wenye kupiga taarabu katika maharusi, na wengine wanaofika hadi kununua kanda (cassettes), CD au Video na kuwapa wenziwao kama zawadi.
 
Watambue wanaoanza kuwahusisha wenziwao na maasi haya kuwa watabeba madhambi yao na ya wenziwao pia na hizo dhambi ataendelea kupata mwenye kuanzisha kila yanaposambaa kwa maelfu ya watu! Ni mzigo mzito kiasi gani atakaoubeba mwenye kumhusisha mwenziwe na maasi haya?

 Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):


 
((إِنَّا نَحْنُ نُحْيِي الْمَوْتَى وَنَكْتُبُ مَا قَدَّمُوا وَآثَارَهُمْ
وَكُلَّ شَيْءٍ أحْصَيْنَاهُ فِي إِمَامٍ مُبِينٍ))  
((Hakika Sisi Tunawafufua wafu, na Tunayaandika wanayoyatanguliza, na wanayoyaacha nyuma. Na kila kitu Tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha))
[Yaasiyn:12]
 
Pia Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametuambia:

 
((من سن في الإسلام سنة حسنة كان له أجرها وأجر من عمل بها من بعده لا ينقص ذلك من أجورهم شيئاً ومن سن في الإسلام سنة سيئة كان عليه وزرها ووزر من عمل بها من بعده لا ينقص من أوزارهم شيئاً)) خرجه مسلم في صحيحه

 
((Atakayefanya kitendo chema katika Uislam atapata ujira wake na ujira wa yule atakayekitenda baada yake bila ya kupungukiwa thawabu zao. Na atakayetenda kitendo kibaya katika Uislam atabeba (mzigo wa) dhambi zake na dhambi za yule atakayetenda wala hapungukiwi kitu katika (mzigo wa) dhambi hizo)) [Muslim]

 
TAHADHARI NDUGU MUISLAMU! BINAADAMU ATAFUFULIWA
NA AMALI YAKE YA MWISHO!


 Ikiwa ndugu yetu Muislamu ni mpenda muziki sana, basi tunakuomba utahadhari na kauli ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliyosema:

 

 
عن جابر بن عبدالله قَالَ : سَمِعْتُ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: (( يُبْعَثُ كُلُّ عَبْدٍ عَلَى مَا مَاتَ عَلَيْه)) رواه مسلم

Kutoka kwa Jaabir bin 'Abdullaah ambaye amesema: "Nimemsikia Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Kila mja atafufuliwa katika hali aliyofia nayo))[Muslim]
 
Je, ndugu Muislamu unayependa muziki, umetafakari vipi utakuwa mwisho wako?

Je, haikuingii khofu katika moyo wako kuwa huenda mwisho wako ukawa ni kuimba nyimbo badala ya kusema "Laa ilaaha Illa Allaah" neno ambalo ukilitaja mwisho wa maisha yako wakati wa kufa utaingia Peponi?

 
KISA CHA KWELI MTU ALIYEFARIKI AKIWA ANASIKILIZA NYIMBO!

Katika moja ya nchi za Ghuba, Kijana mmoja aliyekuwa mpenzi wa nyimbo alikuwa haachi kusikiliza nyimbo katika gari lake. Kila alivyokuwa akikatazwa na wazazi wake na wenziwe waliokuwa wameongoka hakuwa akitaka kusikia nasaha hii. Siku ya ajali yake alitoka akiwa anaendesha gari yake na huku akisikiliza nyimbo ya Ummu Kulthuum 'Hal Ra-al-Hubbu Sukaara' (Je, hakuona mapenzi yanavyolewesha). Alipata maafa mabaya katika ajali hiyo ya gari na ukawa ndio mwisho wake. Kabla ya roho yake kutoka, walijaribu Maaskari wa usalama wa barabarani na waliokuweko kumlakinia (kumsemea atamke 'Laa ilaaha illa Allaah') lakini wapi! Kila akiambiwa aseme 'Laa ilaaha illa Allaah' alikuwa akitamka ''Hal Ra-al-Hubbu Sukaara" "Hal Ra-al-Hubbu Sukaara" na hayo ndio yakawa ni maneno yake ya mwisho akielekea kuonana na Mola wake Mtukufu, na ndio atakayofufuliwa nayo!



Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Aturuzuku mwisho mwema na tunatumai kuwa ndugu zetu ambao bado wako katika maasi haya, watakaposoma dalili hizi, zitakuwa ni mazingatio kwako na kumkhofu Mola wao Mtukufu wajiepusha na uharamu huu na wabaki katika Radhi Zake Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya)

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):
((وَلاَ تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْؤُولاً))

((Wala usifuate (ukipita ukisema au kuyafanya) usiyo na ilimu (ujuzi) nayo. Hakika masikio, na macho, na moyo hivyo vyote vitaulizwa)) [Al-Israa: 36]  

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):
 (( وَلاَ يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا أَيُحِبُّ أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ وَاتَّقُوا اللَّهَ إِنَّ اللَّهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ))
((Wala msisengenyane nyinyi kwa nyinyi. Je! Yupo katika nyinyi anayependa kuila nyama ya nduguye aliyekufa? Mnalichukia hilo! Na mcheni Allaah. Hakika Allaah ni Mwenye kupokea toba, Mwenye kurehemu)) [Al-Hujuraat: 12]
Ibn 'Abbaas (Radhiya Allaahu 'anhuma) amesema: Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ameharamisha Muumimi kumsengenya mwenziwe kama Alivyoharamisha nyamafu.
Maulamaa wamekubaliana kuwa Ghiybah ni haraam kama alivyonukuu Imaam An-Nawawy.
Kauli: 
(( فَكَرِهْتُمُوهُ ))
((Mnalichukia hilo))
kwa maana kama mnavyochukia kula nyama ya ndugu yenu aliyekufa basi vile vile mchukie kumtaja mwenzenu kwa ubaya.

Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):
 ((وَلاَ تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ وَلَا تَنَابَزُوا بِالْأَلْقَابِ بِئْسَ الاِسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الْإِيمَانِ وَمَن لَّمْ يَتُبْ فَأُوْلَئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ))
((Wala msitukanane kwa kabila wala msiitane kwa majina ya kejeli. Ni uovu kutumia jina baya baada ya kwisha amini. Na wasiotubu, hao ndio wenye kudhulumu)) [Al-Hujuraat: 11]

Mwenye kufanya hivyo; mwenye kusengenya na mwenye kumzushia mwenziwe uongo wamelaaniwa na kushutumiwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) katika Aayah ifuatayo:
((وَيْلٌ لِّكُلِّ هُمَزَةٍ لُّمَزَةٍ))
((Ole wake kila safihi, msengenyaji!)) [Al-Humazah: 1]
Ibn 'Abbaas (Radhiya Allaahu 'anhuma) amesema: "Humazah ina maana yule anayetukana na kufedhehesha wenziwe" [At-Twabariy 24: 596] 
Al-Hammaaz:   Mwenye kusengenya kwa vitendo kwa mkono au kwa macho kama kukonyeza.  
Al-Lammaaz: Mwenye kusengenya kwa ulimi (kunena).
[Kauli ya Mujaahid katika Tafsiyr ya Ibn Kathiyr]

Yote hayo ni Ghiybah na adhabu zake ni kama tulivyosoma katika Aayah ya juu hapo; ni mfano wa kula nyama ya ndugu yako aliyekufa. Na pia ni kuonywa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwa 'wayl' ambayo maana yake ni:
1.     Neno la kutisha lenye maana ya kudhalilishwa, kuadhibiwa na kungamizwa.
2.     Ni bonde katika  moto wa  Jahannam

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwa wanaosengenya kwa kuzulia watu maovu,
((إِنَّ الَّذِينَ يُحِبُّونَ أَن تَشِيعَ الْفَاحِشَةُ فِي الَّذِينَ آمَنُوا لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ وَاللَّهُ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ))  
((Kwa hakika wale wanaopenda uenee uchafu kwa walioamini, watapata adhabu iumizayo katika dunia na Akhera. Na Allaah Anajua na nyinyi hamjui)) [An-Nuur: 19].

Monday, June 25, 2012

The Story of Luqman(A.S.) and the Melon

Luqman(A.S.) had great love for the Almighty, that it created within him high moral character and exemplary habits. This was a clear sign of his nobility and nearness to Allah. The details of that is described in Surah(Chapter) Luqman in the Glorious Qur'an.


Luqman(A.S.) used to be in the employ of a rich man. The nobility of Luqman(A.S.)'s character had a great effect on his master, so much so that the master considered him as a great friend and a beloved companion. Although he was the master, yet in fact the master became like a slave to his employee.


It became the practice of the master that whenever he had something special to eat, he would first feed Luqman(A.S.) of it and after Luqman(A.S.) had filled himself, he would eat the left overs. Luqman(A.S.) would consider the love of the master and his habit, so he would eat moderately and send what was left over to the master.


One day, during the melon season, the master received a melon from somewhere. At that time Luqman(A.S.) was not present. The master sent one of his slaves to go and call him. When Luqman(A.S.) arrived, the master cut the melon into slices and slice by slice started giving thereof to Luqman(A.S.) to eat. As he ate the slices, the master inwardly became pleased at the effect his love was having upon Luqman(A.S.).


Luqman(A.S.) ate the slices with great PLEASURE and all the time expressed THANKS for the favour shown to him by the master. After having eaten the slices, when just one slice remained, the master said: "Let me eat this slice and see how sweet is this melon." Saying this, he put the slice into his mouth. Immediately, such bitterness spread from the tip of his tongue down to his throat, that as a result of the extreme bitterness of the meoln, he fell down unconscious and remained unconscious for a whole hour.


When he regained consciousness, he questioned Luqman(A.S.): " O Beloved one, How did you manage to, so heartily eat those slices of melon ? Just one slice of the melon had such an effect on me, then how did you manage to eat so many slices ?" Luqman(A.S.) replied: "O Friend, from your hands I have received hundreds of gifts. The burden of thanks upon me is so great, that my back has gone crooked. Hence, I felt ashamed that the hand that had granted me so much favours, if one day some distastefulness or bitterness should come, how can I turn away from it ? O Friend, the pleasure of knowing that it comes from your hands has changed the bitterness of the melon to sweetness."

Saturday, June 23, 2012

ADHANA USIKU WA MANANE

ADHANA YA USIKU WA MANANE

Mtungaji
Ustadh Shahid Murtadha Mutahhari

Mtarjumi
S. Muhammad Ridha Shushtary


Mchapishaji
Islamic Thought Foundation
No. 5, Takhti Sq., Shahid Beheshti Ave.
P O Box 14155-3899
Tehran, Islamic Republic of Iran
________________________________________
Kimetolewa wavuni na timu ya
Ahlul Bayt Digital Islamic Library Project


ADHANA YA USIKU WA MANANE
________________________________________
Katika zama za ukhalifa wa Bani Umayyah, kabila Ia Kiarabu ndilo kabila la pekee lililokuwa likitawala na lenye nguvu katika dola kuu la Kiislamu. Lakini katika zama za makhalifa wa Bani Abbasi, Wairani walianza kukabidhiwa madaraka na wakadhibiti nyadhifa na vyeo vingi.

Ingawa makhalifa wa Bani Abbasi walikuwa Waarabu, lakini hawakuwa wakiwapenda Waarabu. Siasa yao ilikuwa ni kuwatoa Waarabu madarakani na badala yake kuwaweka Wairani (Waajemi). Isitoshe, walikuwa wakizuia lugha ya Kiarabu isienee katika miji kadhaa ya Iran. Siasa hiyo iliendelea mpaka katika zama za Ma' muun.

Baada ya kufa kwa Ma'muun, ndugu yake, Mu'tasim, akakalia kiti cha ukhalifa. Ma'muun na Mu'tasim walikuwa ndugu baba mmoja lakini mama zao walikuwa mbalimbali. Mamake Ma'muun alikuwa Mwajemi (Mwirani) na mamake Mu'tasim alikuwa Mturuki. Hii ndiyo sababu iliyowafanya Wairani ambao walikuwa wameshikilia vyeo muhimu - wasiupende uldialifa wa Mu'tasim. Wairani walitaka Abbas mwana wa Ma'muun awe khalifa. Mu'tasim alitambua jambo hili na akawa akiogopa asije mtoto wa nduguye - Abbas bin Ma'muun - akaasi na kwa msaada wa Wairani akamwangusha. Kwa hivyo akapanga njama ya kumwangamiza Abbas na kuvunja nguvu za Wairani ambao walikuwa wakimwunga mkono Abbas. Akamtia jela Abbas ambapo ndipo alipokufa. Ili kuvunja nguvu za Wairani, akafanya mpango wa kuwapa nguvu watu wengine badala yao. Kwa ajili ya kutekeleza mpango huo, akawaleta Baghdad (makao makuu ya ukhalifa) Waturuki wengi wa kabila la mama yake kutoka Uturuki (Turkistan) na Maa Waraun Nahr na akawapa kazi. Haukupita muda mrefu, Waturuki wakashika madaraka na nguvu zao zikazidi kuliko Waarabu na Wairani.

Kwa kuwa Mu'tasim alikuwa akiwaamini sana Waturuki hivyo, kila siku zikipita alikuwa akiwapa uwanja; na kutokana na siasa hiyo Waturuki wakawa ni watu wa pekee wenye nguvu katika dola la Kiislamu. Waturuki wote walikuwa Waislamu, walijifunza lugha ya Kiarabu na walikuwa waaminifu kwa dini ya Kiislamu, lakini ilivyokuwa muda baina ya kuingia kwao katika mji mkuu wa ustaarabu wa Kiislamu na kupata madaraka haukuwa mrefu, hawakuelewa sana mafundisho, adabu na utamaduni wa Kiislamu na hawakuwa na mwendo na tabia ya Kiislamu. Kinyume chake, Wairani walikuwa na uzoefu wa ustaarabu na walijifunza kwa hamu maarifa, maadili na adabu za Kiislamu, mwendo wao ulikuwa wa Kiislamu na walikuwa mbele katika kuutumikia Uislamu. Katika kipindi ambacho Wairani walikuwa na madaraka mikononi mwao, Waislamu wote waliridhika; lakini wakati Waturuki waliposhika madaraka waliwatendea vibaya Waislamu kwa kadiri kwamba walikuwa wakichukiwa.

Askari wa Kituruki wenye kupanda farasi walipokuwa wakipita kwenye mitaa na vichochoro vya Baghdad hawakuwa wakitazama kama yupo mtu mbele ya njia yao. Kwa sababu hiyo, mara nyingi wanawake, watoto, wazee na watu wasiojiweza walikuwa wakikanyagwa na farasi. Watu hawakuweza kustahamili udhalilifu huo. Wakamwomba Mu'tasim ahamishe mji mkuu kutoka Baghdad na afanye mahali pengine. Katika maombi yao walisema kwamba ikiwa khalifa hatohamisha mji mkuu basi watapigana vita dhidi yake. Mu'tasim akawajibu: "Nguvu gani mlizonazo mtakazoweza kupigana dhidi yangu? Mimi nina askari thamanini elfu waliojiandaa kwa silaha." Watu wakamjibu: "Tutapigana kwa mishale ya usiku, yaani tutakupiga kwa laana za usiku wa manane." Mu'tasim akakubali maombi ya watu baada ya kusikia maneno hayo. Akahama Baghdad na akafanya Samarah kuwa ni mji wake mkuu. Baada ya Mu'tasim, Waturuki waliendelea kushika madaraka katika zama za ukhalifa wa Wathiq, Mutawakkil, Muntasir na makhalifa kadhaa wengineo. Waturuki walikuwa wakiwatumia makhalifa hao kwa maslahi yao. Baadhi ya makhalifa wa Bani Abbasi walijaribu kuvunja nguvu za Waturuki lakini walishindwa. Khalifa mmojawapo wa Bani Abbasi aitwaye Mu'tadhid, ndiye aliyeweza kwa kadiri fulani kupunguza nguvu za Waturuki.

Katika zama za Mu'tadhid, alikuwepo mfanyabiashara mmoja mzee ambaye alikuwa akimdai pesa nyingi afisa mmoja wa kijeshi lakini alikataa kumlipa. Mwishowe akaamua amwendee khalifa mwenyewe aingilie kati, lakini kila wakati alipofika kwenye mlango wa kasri ili apate kuonana na khalifa, mabawabu na watumishi wa kasri walikuwa wakimzuia.

Mfanyabiashara maskini alivunjika moyo na hakujua afanye nini. Kwa bahati mtu mmoja akamwelekeza aende kwa mshoni wa nguo katika gulio, na akamwambia kwamba mtu huyo ndiye atakayeweza kumsaidia. Mfanyabiashara akaenda kwa mshoni ambaye alimwamuru afisa huyo wa kijeshi amlipe deni yake. Mfanya biashara akalipwa pesa zake bila ya kukawia.

Kitendo hicho kilimshangaza sana mfanya biashara mzee. Akamshikilia sana mshoni kwa kumwuliza: "Vipi Waturuki hao ambao hawamjali mtu yeyote wanatii amri yako?"

Mshoni akajibu "Mimi nina kisa kimoja ambacho ni lazima nikuhadithie wewe. "Siku moja nilipokuwa nikipita katika njia moja, wakati huohuo mwanamke mmoja mrembo alikuwa akipita hapo. Kwa bahati, afisa mmoja Mturuki ambaye alikuwa amelewa alikuwa ametoka nje ya nyumba yake na akasimama mlangoni akiwatazama watu wanaopita njiani. Alipomwona huyo mwanamke mrembo akapandwa na wendawazimu, akamkumbatia mbele va watu kisha akamvuta kumtia nyumbani kwake. Mwanamke huyo akaanza kupiga mayowe: 'Enyi watu! Nisaidieni! Mimi si mzinzi! Nina heshima zangu! Wallahi ikiwa usiku mmoja nitalala nje, mume wangu atanitaliki! Unyumba wetu utaharibika!'

"Hakuna mtu aliyethubutu kusogelea mbele kumsaidia kwa kuogopa. Mimi nikamwendea na kwa upole sana nikamwomba afisa amwache mwanamke, lakini akanijibu kwa kunipiga kwa nguvu rungu ya kichwa na kunipasua, kisha akamtia mwanamke ndani ya nyumba yake. Mimi nikawakusanya watu wachache, kisha kwa pamoja tukaenda kwenye nyumba ya afisa huyo kutaka amwachie mwanamke, lakini mara afisa Mturuki akatoka nyumbani pamoja na kikundi cha watumishi na watumwa wake na wakaanza kutupiga magongo.

"Sote tukakimbizana na mimi nikarejea nyumbani, lakini kila wakati nilikuwa nikimfikiria mwanamke huyo maskini. Nikafikiri kwamba ikiwa mwanamke huyo atabaki na mwanamume huyo mpaka asubuhi, basi maisha yake yote mpaka kufa kwake yataharibika na hatoweza tena kurejea nyumbani kwake. Nilikaa macho nikifikiri mpaka nusu ya usiku. Mara mpango mmoja ukanijia ubongoni mwangu. Nikasema moyoni. 'Mwanamume huyo amelewa leo usiku na hatambui wakati. Ikiwa nitaadhini sasa hivi, atadhani kuwa ni alfajiri, hivyo atamwachia mwanamke. Mwanamke pia ataweza kurejea nyumbani kwake kabla ya kupambazuka.

"Kwa haraka nikaenda msikitini, nikapanda mnarani na nikaadhini kwa sauti kubwa. Nilipokuwa nikiadhini nilikuwa nikiangalia njiani kuona kama mwanamke ameachiwa ama la. Mara ghafla, niliwaona askari wengi waliopanda farasi na waendao kwa miguu wakimiminika njiani huku wakiulizana: 'Ni nani huyo aliyeadhini wakati huu wa usiku?' Mimi juu ya kuwa niliogopa sana, nikajitambulisha: 'Mimi ndiye niliyeadhini.'

"Wakasema: 'Teremka chini haraka unaitwa na khalifa!' "Wakanichukua kwa khalifa. Nikamkuta khalifa ameketi akiningojea. Akaniuliza: 'Kwa nini umeadhini wakati huu wa usiku?' Nikamwelezea kisa chenyewe tangu mwanzo mpaka mwisho. Papo hapo, khalifa akatoa amri kwamba afisa na mwanamke waletwe mbele yake. Baada ya kuletwa mbele yake na kuwahoji, akatoa amri afisa huyo auawe. Mwanamke akapelekwa nyumbani kwa mumewe na akamtaka asimlaumu bali amwangalie vizuri kwa sababu khalifa ana hakika kwamba mwanamke hakuwa na kosa lolote.


"Kisha Mu'tadhid akaniambia: 'Wakati wowote utakapoona uonevu kama huo, tumia mbinu hiyo mpya uliyoitumia, nami nitachunguza.' "Habari hii ikaenea kwa watu wote. Tangu siku hiyo hao [Waturuki] wakaanza kuniogopa. Hii ndiyo sababu kwamba nilipomwamrisha huyo afisa wa kijeshi akulipe pesa ulizokuwa ukimdai, alitii haraka." Adhana Usiku wa Manane

Monday, June 18, 2012

ISRAA WA MIRAAJ



Mara baada ya kurudi katika safari ya Miraji aliyopelekwa ndani yake mpaka mbingu ya saba, kisha akasogezwa mahali panapoitwa ‘Sidratul muntaha na kuzungumza na Mola wake Subhahanu wa Taala, kisha akarudishwa ardhini katika usiku huo mmoja, na kabla ya kumhadithia mtu yeyote juu ya safari yake hiyo adhimu, Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa amekaa kimya nje ya msikiti wa Al Kaaba, na Abu Jahal alipomuona katika hali ile akamuendea na kuanza kumkejeli huku akimuuliza.
"Enhe! Vipi pana habari yo yote mpya kutoka mbinguni leo?"
Kwa utulivu na upole Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamjibu: "Ndiyo, nilipelekwa usiku wa leo mpaka Baitul Maqdis (Palestina)."
Abu Jahal: "Na asubuhi hii ukarudi Makkah?"
Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): "Naam, na nilisali na ndugu zangu Manabii huko."
Abu Jahal akapiga ukelele kama mwenda wazimu na kuwaita jamaa zake.
"He! Amma leo Muhammad ametia fora"
Akaanza kuwahadithia yale aliyoyasikia kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), jambo lililowafanya hata baadhi ya waliosilimu karibuni wastushwe na habari hizo na kurudi nyuma kidogo.
Washirikina wa Kikureshi wakaona kuwa leo ndiyo siku ya kumfedhehesha Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na kumtenganisha na sahibu yake Abubakar (Radhiya Allaahu ‘anhu), wakaanza kusemezana;
"Abubakar anajua kuwa inachukua miezi mingi kusafiri kutoka Makkah hadi Sham, mahali ulipo msikiti huo wa Baytul Maqdis, maana kesha safiri kwenda huko mara nyingi, na leo Muhammad anasema eti amesafiri hadi huko ndani usiku mmoja tu"
Wakenda mpaka nyumbani kwa Abubakar (Radhiya Allaahu ‘anhu) na kumgongea mlango huku wakimwita kwa sauti kubwa: "Abubakar!",
Abubakar  (Radhiya Allaahu ‘anhu) akauliza: " Kuna nini tena?"
Makureshi: "Rafiki yako Muhammad …"
Abubakar (Radhiya Allaahu ‘anhu): "Amefikiwa na jambo lolote?"
Makureshi:" "Eti anasema kuwa amesafiri usiku wa leo kutoka Makkah hadi Baytul Maqdis na kurudi."
Abubakar  (Radhiya Allaahu ‘anhu): "Ni yeye Mwenyewe aliyesema hayo?"
Makureshi: " Ndiyo! Tena tumemsikia kwa masikio yetu!"
Abubakar (Radhiya Allaahu ‘anhu): "Ikiwa Yeye Mwenyewe amesema hivyo, basi mimi namsadiki. Mimi namsadiki kwa mambo makubwa kupita hayo. Nasadiki kuwa anapata Wahyi unaotoka mbinguni, basi nisimsadiki juu ya kwenda hapo Baytul Maqdis?"
Hii ndiyo Imani ya Abubakar (Radhiya Allaahu ‘anhu) ambayo ikiwekwa upande mmoja wa mizani na zikiwekwa Imani za watu wote upande wa pili, basi imani ya Abubakar (Radhiya Allaahu ‘anhu) itazidi uzito.
Abubakar (Radhiya Allaahu ‘anhu) akavaa nguo zake, akatoka na kwenda kumtafuta Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), aliyemkuta amekaa kimya peke yake nje ya Al Kaaba, akamsogelea na kumkabili, kisha kwa utulivu na khushuu akamkumbatia na kumwambia;
"WAllaahi wewe husemi uwongo na mimi nakusadiki , WAllaahi nakusadiki."

Thursday, June 14, 2012

حق الزوجه على زوجھا Haki Za Mke Juu Ya Mume


بسم لله الرحمن الرحي
Alhamdulillaahi Rabil-´Aalamiyn, swalah na salaam zimwendee mja wake na Mtume Wake Muhammad (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na ahli zake na Maswahaba wake (radhiya Allaahu ´anhum). Amma ba´ad:
Hakika Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) Kaumba mume na mke kutokana na hekima kubwa. Lau kusingelipatikana ila mwanaume tu, au kusingelipatikana ila mwanamke tu, kungekuwepo kasoro nyingi kwa kila mmoja na kusingelipatikana utulivu. Hili lamuhusu mwanaadamu. Hali kadhalika kwa viumbe vingine vyote.
وَمِن كُلِّ شَيْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ
”Na katika kila kitu Tumeumba kwa jozi ilimzingatie.” (51:49)
وَالَّذِي خَلَقَ الْأَزْوَاجَ كُلَّھَا
”Na Ambaye ndiye Aliyeumba katika kila kitu jike na dume.” (43:12)
Hakika Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) Kafanya hili kwa hekima kubwa. Lakini Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) Kamkirimu mwanaadamu.
وَلَقَدْ كَرَّمْنَا بَنِي آدَمَ
”Na hakika tumewatukuza wanaadamu.” (17:70)
Kamkarimu zaidi ya viumbe vingine vyote. Na katika ikram za Allaah kwa mwanaadamu ni kuwa hakumwacha hovyo kama wanyama ambao wanaingiliana wao kwa wao wanaume kwa wanawake kwa ajili ya kujitoa matamanio tu, kisha wanafarakana na wala hawajuani baadhi yao, na wala hawana nyumba na jamii. Ila Allaah Kamkarimu mwanaadamu kwa mengi, na katika hayo ni pale Aliposema:
وَللهُّ جَعَلَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِكُمْ أَزْوَاجًا وَجَعَلَ لَكُم مِّنْ أَزْوَاجِكُم بَنِينَ وَحَفَدَةً وَرَزَقَكُم مِّنَ الطَّيِّبَاتِ
”Na Allaah Amekuumbieni wake katika jinsi yenu, na Akakujaalieni kutoka kwa wake zenu wana na wajukuu, na Akakuruzukuni vitu vizuri vizuri.” (16:72)
Hizi ni katika neema za Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) kwa mwanaadamu.
Hekima ya ndoa katika Uislamu ni kubwa na pia ni kujilinda na tabia mbaya, zinaa na kufanya machafu. Kwa kuoa, mtu hujilinda na mambo haya kwa idhini ya Allaah – kwa watu wa iymaan; ama makafiri na watu wanaofuata matamanio hawa hawazingatiwi. Ama kwa watu wa iymaan wanapata utulivu kwa hilo.
وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِّتَسْكُنُوا إِلَيْھَا وَجَعَلَ بَيْنَكُم مَّوَدَّةً وَرَحْمَةً
”Na katika Ishara Zake ni kuwa Amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye Amejaalia mapenzi na huruma baina yenu.” (30:21)
Hii ni katika hekima kubwa ya Allaah Kujaalia baina ya mume na mke mapenzi na huruma, ili wasifarakane na wasichokane.
Hakika mwanamke ana haki zake juu ya mume wake.
Ya kwanza ni juu yake kumhudumia, matumizi ni kwa mwanaume na siyo mwanamke. Mwanamke hamhudumii (hampi matumizi) mwanaume. Bali matumizi ni kwa mwanaume yeye ndiye humhudumia mwanamke.
الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاء بِمَا فَضَّلَ للهُّ بَعْضَھُمْ عَلَى بَعْضٍ وَبِمَا أَنفَقُواْ مِنْ أَمْوَالِھِمْ
”Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa kufadhiliwa na Allaah baadhi yao juu ya baadhi, na kwamali yao wanayo yatoa.” (04:34)
Na alipokuja Hind kwa Mtume wa Allaah ( صلى لله عليه وسلم ) akimshtaki mume
wake kuwa hawapi matumizi yakuwatosheleza na yanawatosha watoto wake
tu. Akamwambia Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) chukua kinachokutosheleza kwa
wema. Akamwambia Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) achukue matumizi yake kwa
mume ikiwa ni bakhili, atachukua mke matumizi yatayomtosheleza yeye na
watoto wake.
Hii ni wajibu kwako. Na si pendekezo, bali ni haki wajibu juu yake [mume]. Na matumizi inatakikana iwe kwa wema, kwa mambo yanayojulikana na watu katika kila zama na mahala. Tajiri ana matumizi yake na fakiri ana matumizi yake, na mtu wa kati na kati ana matumizi yake. Hii ni katika haki ya mke juu ya mume wake, matumizi kwa wema. Amsimamie kumpa matumizi yake.
Na wala siyo lazima mwanamke ashiriki katika [kusaidia] matumizi, hata akiwa na mali nyingi si lazima kwake kutoa kitu katika matumizi ila kwa kupenda kwake mwenyewe. Kwa kuwa matumizi yake ni wajibu kwa mume kwa mujibu wa ndoa, na kwa mujibu wa mkatabaulio baina yao. Na hili ni katika Alilomfadhilisha Allaah mwanaume zaidi kuliko mwanamke. Ni kule suala la matumizi likawa jukumu la mume na si mwanamke.
Hali kadhalika utulivu, haki ya mke juu ya mume wake ni kumpa utulivu utaoleta amani na pozo.
Katika haki za mke juu ya mume wake kumkatia nguo inayomfaa khasa wakati wa sherehe n.k, katika mavazi wanayovaa wanawake katika mji huo. Na mambo haya ni katika haki za mke juu ya mume wake. Matumizi, utulivu na kumkatia nguo. Na ikiwa mume hawezi mambo haya, hapo mwanamke ana khiyari aidha ya kubaki na kuvumilia hali hii - Alhamdulillaah, na akitaka kufarakana naye anaacha naye. Ili kumuondolea madhara mwanamke. Hizi ni katika haki za Uislamu ilizompa mwanamke.
Katika haki za mke juu ya mume wake, ni kumlinda na haramu - kwakumjamii kadiri na atavyoweza. Na hili ni katika kusudio kubwa la ndoa. Mwanamke kumlinda mwanaume na mwanaume kumlinda mwanamke. Ama mume akimtenga na hawana maingiliano yoyote, hili litaleta madhara. Akitaka mwanamke kusubiria hali hii sawa, la sivyo wafarakane ili kujiondolea madhara ikibainika kuwa mume hana uwezo wa kujimai.
Katika haki za mke juu ya mume wake; ni pale mume atapotaka kuoa mwanamke wapili, au watatu au wanne - ana ruhusa ya hilo. Allaah Kamruhusu. Mwanamke awe radhi kwa hilo kwa kuwa hili ni jambo kamruhusu nalo Allaah. Kama Alivyosema Allaah (Ta´ala):
فَانكِحُواْ مَا طَابَ لَكُم مِّنَ النِّسَاء مَثْنَى وَثُلاَثَ وَرُبَاعَ
“Basi oeni mnaowapenda katika wanawake, wawili au watatu au wane.” (04:03)
فَإِنْ خِفْتُمْ أَلاَّ تَعْدِلُواْ فَوَاحِدَةً
“Na mkiogopa kuwa hamwezi kufanya uadilifu, basi mmoja tu.” (04:03)
Ama mkijiamini katika nafsi zenu kusimama na uadilifu - ukifanya uadilifu, ukitaka hilo ni ruhusa kwako au ni mwenye haki ya hilo. Na hili la ukewenza lina maslahi makubwa katika jamii, [maslahi] kwa wanawake. Maslahi ya ukewenza ni zaidi kwa wanawake kuliko maslahi yanayopatikana kwa waume. Kwa kuwa mume ndiye mwenye kuchukua jukumu la kupambana na baadhi ya hao wake zake; kila mmoja ampe matumizi, kumkatia nguo, makazi na mengineyo.
Isitoshe wanawake katika kila jamii ndio wengi zaidi kuliko wanaume, kila mwanaume akibaki kuoa mke mmoja kutabakia wanawake wengi sana. Kutokana na rahma ya Allaah [kwa wanawake] Akaweka katika Shari´ah ukewenza, kwa ajili ya kuondosha uchafu na wanawake [wasiyokuwa na waume] kuwa wengi. Lau mume ataishia kuoa mwanamke mmoja wanawake watakuwa wengi katika jamii, na ufisadi utaenea kunako tabia. Mwanamke ni mwenye haja ya ataemsimamia, atamlisha, kumtetea. Yeye ni mwenye haja ya mume.
Hivyo hekima ya ukewenza ni kubwa. Wale wanaopinga ukewenza - wanasema kuwa hii ni dhuluma kwa mwanamke. Hili ni kutokana na ufahamu wao mbaya au ni kutokana na ´Aqiydah [itikadi] yao mbovu. Bali la ukewenza lina khayr nyingi kwa wanawake na si kwa wanaume.
Kwa kuwa maslahi ya ukewenza kwa wanawake ni makubwa kuliko maslahi wanayopata wanaume. Kwa kuwa wanawake ndiyo wenye haja kubwa kwa wanaume kuliko wanaume. Na ni bora kwa mwanamke kuolewa na mume aliye na wake wanne; na mume anaemsimamia kwa mahitajio yake na anamhifadhi, anakuwa mahram wake, na huenda Allaah Akawaruzuku
watoto. Haya maslahi ni bora kuliko kubaki bila ya kuwa na mume. Hata akiwa ni mwanamke wanne. Jambo la ukewenza katika Uislamu lina hekima kubwa.
Hawa wanaopinga ukewenza na wanasema kuwa ni dhuluma kwa mwanamke, huku ni kujidanganya na kuwa na ufahamu mbaya. Au ni upotofu! Subhaana Allaah! Wanaruhusu uzinzi na wanapinga ndoa ya Kishari´ah! Hizi ndizo dini za kijaahiliyyah na dini ya kinaswara ambao nao wanapinga ukewenza. Wanapinga ndoa ya Kishari´ah nzuri na wanaenda kufanya uhuni wa kila ainanje. Mwanaume na mwanamke wanafanya wapendacho ila tu wasifanye ndoa, kisha wanaita [ukewenza] ndiyo uchafu!! Uchafu ni kwao - A´udhubillaah. Na huku ni katika kubadilisha maumbile. Na wao wanataka waislamu wawe hivyo. Na waumini hawataki hilo.
Hivyo mume akitaka kuongeza mke hana kipingamizi, si kwa hakimu, si kwa mke wake wala kwa walii wa mke. Kwa kuwa hili ni jambo kamruhusu nalo Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala), na hili ni kutokana na maslahi ya jamii. Hana kipingamizi. Isipokuwa tu ikiwa mwanamke alimuwekea sharti wakati wa ndoa asioe mwengine, alimuwekea sharti asioe mwengine; tunasema hili haliwezi kuzuia yeye kuoa, hata kama mwanamke alimuwekea sharti haliwezi kumzuia kuoa. Kwa kuwa hili ni jambo kamruhusu Allaah na wala hakuna yeyote awezae kumkataza. Lakini mwanamke ana khiyari, akio mwanamke mwengine ana khiyari. Akitaka atabaki naye na akitaka ataomba kufarakana naye. Ana khiyari aidha ya kubaki au kufarakana. Lakini mwanamke ana khiyari, akioa mwanamke mwengine ana khiyari. Akitaka atabaki naye na akitaka ataomba kufarakana naye. Ana khiyari aidha ya kubaki au kufarakana. Kwa kuifanyia kazi kauli ya Mtume (´alayhis-Salaam):
"Waislamu wako kwa masharti yao [wanayowekeana]."
Lakini si katika sharti yake [mwanamke] kumkatalia kuoa, hapana ni haki
yake. Lakini akitaka kutengana naye ataenda mahakama na athibitishe kama
kweli alimuwekea sharti, halafu hapo yeye ndio atakuwa na khiyari. Ima
abaki naye au wafarakane kwa kuifanyia kazi sharti.Lakini ukewenza
alioruhusu Allaah Kauwekea sharti la mtu kufanya uadilifu baina ya wake
wawili.
فَإِنْ خِفْتُمْ أَلاَّ تَعْدِلُواْ فَوَاحِدَةً
“Na mkiogopa kuwa hamwezi kufanya uadilifu, basi mmoja tu.” (04:03)
(Allaah) Akaweka sharti ya ukewenza, mtu afanye uadilifu baina ya wake zake.
Na uadilifu ni kufanya nini?
Uadilifu alioweka Allaah ni ule unaowezekana; uadilifu katika matumizi, utulivu, kumkatia nguo, kitandani kuwagawia siku sawa. Na haijuzu huku walala siku kadhaa kwengine chini ya hapo. Haijuzu kufanya hivi. Lazima wote uwagawie siku sawa. Huu ndiyo uadilifu unaotakikana. Wanawake lazima watendewe haki sawa katika matumizi, utulivu, kuwakatia nguo na siku za kulala.
Ama mapenzi ya moyoni ukampenda mmoja zaidi kuliko mwengine, hili halimiliki yeyote ila Allaah (Jalla wa ´Alaa). Mume anaweza kuwapenda baadhi ya wake zake zaidi kuliko wengine, yaliyo moyoni yanamilikiwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Hili mume hakalifishwi. Si katika sharti kuwapenda wote sawa, hutoweza. Huwezi kugawa mapenzi baina ya wake sawa sawa, hili liko kwenye Mkono wa Allaah (Jala wa ´Allaa). Na kutokana na hili Kasema Allaah (Jalla wa ´Alaa) katika Aayah nyingine:
وَلَن تَسْتَطِيعُواْ أَن تَعْدِلُواْ بَيْنَ النِّسَاء وَلَوْ حَرَصْتُمْ فَلاَ تَمِيلُواْ كُلَّ الْمَيْلِ فَتَذَرُوھَا كَالْمُعَلَّقَةِ
“Wala hamtaweza kufanya uadilifu baina ya wake, hata mkikakamia. Kwa hivyo msimili moja kwa moja mkamwacha (mmojapo) kama aliye tundikwa.” (04:129)
Mahaba na mapenzi ya moyoni haya yako kwenye Mkono wa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Lakini mume asimili kwa mke mmoja akadhihirisha [wazi wazi] kuwapenda baadhi ya wake zake zaidi kuliko wengine, akawapendelea wao na kumdhulumu wapili. Akampa vingi zaidi kuliko yule asiempenda. Akampa matumizi mengi, kumuweka katika makazi mazuri [kuliko mwengine], hili halijuzu. Kumilia. Analala kwa yule ampendae siku nyingi zaidi ya yule asiempenda, huku ni kumilia. Na imekuja katika Hadiyth:
"Yule mwenye wake wawili, akamkandamiza mmoja zaidi kuliko mwengine, atakuja siku ya Qiyaamah na bega lake likiwa limepinda."
Itakuwa ni fedheha kwake - Allaah Atukinge. Na malipo yanatokana na chanzo cha amali. Haya ni makemeo makali.
Tumejifunza katika haya kuwa uadilifu umegawanyika namna mbili, uadilifu unaowezekana na ndiyo alioutaja Allaah (Ta´ala):
فَإِنْ خِفْتُمْ أَلاَّ تَعْدِلُواْ فَوَاحِدَةً
“Na mkiogopa kuwa hamwezi kufanya uadilifu, basi mmoja tu.” (04:03)
Na audilifu usiowezekana. Na huu ndio uliousema Allaah (Ta´ala):
وَلَن تَسْتَطِيعُواْ أَن تَعْدِلُواْ بَيْنَ النِّسَاء وَلَوْ حَرَصْتُمْ
“Wala hamtaweza kufanya uadilifu baina ya wake, hata mkikakamia.” (04:129)
Makusudio ni ulaini wa moyo na mapenzi ya moyo, hili liko kwenye Mkono wa Allaah. Lakini asimili ikiwa anapenda baadhi ya wake zaidi kuliko mwengine, asidhihirishe hilo ikawa anampendelea mmoja na anamkandamiza mwengine kunako haki zake. Uwezo wa kuwapa matumizi, utulivu na mavazi sawa unamiliki haya, haya unayaweza. Na kutokana na hili Akasema:
فَلاَ تَمِيلُواْ كُلَّ الْمَيْلِ
“Kwa hivyo msimili moja kwa moja.” (04:129)
Yaani akamili mapenzi ya moyoni na mapenzi ya matendo. Huku ndio kumili moja kwa moja.
فَتَذَرُوھَا كَالْمُعَلَّقَةِ
“(Mmojapo) akawa kama aliye tundikwa.” (04:129)
Hajulikani ana mume na isitoshe siyo mwenye kutalikika. Ni dalili kuwa kilichokatazwa ni kumili moja kwa moja, ama kulimi kidogo nako ni kumili kwa [mapenzi ya] moyo, hili haliko katika uwezo wa binaadamu. Anaweza kuwapenda baadhi ya wake zake zaidi kuliko wengine. Mapenzi hili linatokana na Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala), na [mapenzi ya] moyo yako kwenye Mkono wa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Sisi tumekalifishwa kwa yale tunayoweza.
Hizi ni katika haki za mke juu ya mume wake, akioa mwanamke mwengine - wapili, watatu au wanne afanye uadilifu kwa mambo yanayowezekana kufanya uadilifu. Kwa kuwa baadhi ya watu wengi, na hili hutokea sana; wanapooa mwanamke, anamfanyia uadilifu yule mwanamke mpya tu na anamwacha mwanamke wakwanza, hataki kuongea naye, anamdhulumu na anamuona mbaya; kana kwamba ni dhalimu na ni mujrima [mwanamke huyu]. Hili halijuzu katika Uislamu. Bi mkubwa na bi mdogo wote ni sawa kunako haki. Si kwamba mwanamke akiwa mkubwa anakuwa na haki zaidi, na anakuwa mwanamke mjane ana haki zaidi ya yule mkubwa, hapana! Haki ni zile zile kwa mkubwa na bi mdogo maadamu wako katika khidima yako. Ila tu ikiwa mwanamke atachagua kubaki nawe katika hali hi [mume akawa si mwadilifu], uamuzi ni wake.
Na kutokana na hili Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) alipotaka kumtaliki Sawdah bint
Zam’ah (radhiya Allaahu ´anha), aliomba kutoka kwa Mtume ( ( صلى لله عليه وسلم
kubaki katika khidma yake na kubaki naye na kusamehe haki yake kumpa
´Aaishah.
Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) akamkubalia hilo. Hivyo mwanamke akiridhia
kubaki hata kama mume wake hamjamii nakadhalika, akiridhia ni haki yake.
Na ikiwa hayuko radhi kwa hilo ana haki ya kuomba wafarakane. Au ikiwa
yeye [mume] hana matamanio kwa mwanamke [huyo], asimwache akabaki
kama aliye tundikwa. Akitaka kubaki na watoto wake na nyumba yake nawe
uko katika hali hiyo, hakuna neno. Na kama hawezi, hii ni haki yake.
Ama [mwanaume] hamjali kabisa naye kashughulishwa tu na huyo
mwanamke mpya kama kwamba yule mwanamke wakwanza ni adui na
mujrima, hii ni dhuluma. Na hili ndilo alilolielezea Mtume ( ( صلى لله عليه وسلم
kuwa atakuja simu ya Qiyaamah na bega lake likiwa limepinda, hii ni fedheha
kwake kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).
Ni wajibu kwa wanaume wamche Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) katika mambo haya na wasitumie udhaifu wa wanawake kwa kuwadhulumu au kuwanyima haki zao khasa ikiwa mwanamke anakereka na hawezi kujitetea na wala hana pakukimbilia, ni wajibu kwa mwanaume kuwa naye vizuri na kumpa haki zake anazopaswa maadamu yuko katika khidma yake. Ampe haki zake. Na ajue akibaki [mwanamke] katika khidma yake na akamuacha na kumtenga na kutomjali, atahesabiwa kwa hayo siku ya Qiyaamah na atahesabika ni katika wenye kudhulumu siku ya Qiyaamah. Amuamrishe swalaha, amuamrishe kumtii Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala), amkataze munkari, asitoke ila kwa adabu za Kishari´ah. Hizi ni katika haki za mke juu yake [mume]. Yeye ni mchungaji kwake.Anasema Allaah (Ta´ala):
يَا أَيُّھَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَھْلِيكُمْ نَارًا وَقُودُھَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ
“Enyi mlioamini! Jilindeni nafsi zenu na ahali zenu na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe.” (06:66)
Miongoni mwa ahli, ni mke wako. Kama jinsi unavyoihofia nafsi yako na moto, ni wajibu vile vile kuwahofia ahali zako na moto. Anasema (Subhaanahu wa Ta´ala):
وَأْمُرْ أَھْلَكَ بِالصَّلَاةِ وَاصْطَبِرْ عَلَيْھَا
“Na waamrishe watu wako kusali, na uendelee mwenyewe kwa hayo.” (20:132)
Na Anasema kuhusiana na Mtume Ismaa´iyl (´alayhis-Salaam):
وَكَانَ يَأْمُرُ أَھْلَهُ بِالصَّلَاةِ وَالزَّكَاةِ وَكَانَ عِندَ رَبِّهِ مَرْضِيًّا
“Na alikuwa akiwaamrisha watu [ahli] wake Swalah na Zakaah, na alikuwa mbele ya Mola Wake mwenye kuridhiwa.” (19:55)
Katika haki za mke juu ya mume wake ni kumshaji´isha katika khayr na amkataze na shari na amkanye aonapoanatoka katika utiifu wa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Na wala asimwachie uhuru; akamwachia akatoka apendavyo, akaongea kwenye simu na ampendae, akaenda sehemu za kipuuzi au akaenda kwenye hafla zisizo na heshima, hafla za harusi zisizo na heshima na zenye munkari - akamwacha. Yeye ni msimamizi juu yake, ni mchungaji. Na hii ni katika haki ya mke juu yake mume, kwa kuwa huyu ni mwanamke na hajui maslahi yake. Ni juu yake amsimamie na kumwangalia. Na huku ni kumkarimu.
Kwa kuwa baadhi ya watu wanafikiri kumkarimu mwanamke ni kumpa uhuru wake, huku siyo kumkarimu bali ni katika kumdhuru. Ni juu ya mwanaume kujua kuwa ni msimamizi wa mke wake. Kila mukhaalafah [kupinda] kwake, ataulizwa na Allaah kwa nini hakumuamrisha, hakumkataza, hakumuelekeza na wala hakumkataza kwa mambo yasiyompasa. Na hii ni katika ya mke juu ya mume. Haki juu yake si kumlisha na kumnywesha na kumpa mavazi tu, hizi ni haki lakini hazitoshi. Haki kubwa ni kumsimamia na kumlazimisha kumtii Allaah na kumkataza na kumuasi Allaah. Hii ni katika haki kubwa kwake [mume]. Na walii wake [mkeo] kakupa mtoto wake kama amana kwa dhima yako.
Walii wake hajui chochote kuhusiana naye. Wewe ndiye utaulizwa kuhusiana na yeye [mke] na ni amana uliopewa. Na Mtume (´alayhis-Salaam) katika Hijah [ya mwisho] ya kuaga anasema:
"Ninawausia kuwatendea wanawake khayr [wema]. Kwani wao ni wafungwa wenu." (Ibn Maajah (1851))
Mwanamke ni mfungwa kwa mume wake. Ni wajibu kwake mume kuwa naye vizuri mke huyu na mfungwa huyu, amuongeleshe vizuri, amtendee mazuri na amchukulie mke wake ni mtu mwenye hadhi na cheo chake, pozo la maisha yake na mama wa watoto wake na msimamizi wa nyumba yake. Awe naye vizuri na kumchunga vizuri, hili ndilo linalotakikana. Na wajibu mkubwa kwa mume ni kumlinda mwanamke na yasiomstahiki. Na awe msimamizi wake. Kama Alivyosema Allaah (Jalla wa ´Alaa):
الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاء بِمَا فَضَّلَ للهُّ بَعْضَھُمْ عَلَى بَعْضٍ
“Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa kufadhiliwa na Allaah baadhi yao juu ya baadhi.” (04:34)
Kwa sababu baadhi ya wanaume hawana usimamizi, badala yake wao ndio wakwanza kumharibu mke kwa kumuwekea TV, dish nk; Haya ni madhara ewe ndugu, haya si katika mashali yake na wala katika haki za mke juu yako mume, bali ni kumuwekea madhara.
Ni wajibu kwa wanaume kuzingatia haya, na wajue kuwa mke ni amana kuanzia pale alipomuongelesha kwa walii wake. Ni wajibu kwake kumwangalia na kumkarimu na asimame kwa haki ambazo ni wajibu juu yake.

Haki Za Mume Juu Ya Mke

حق الزوج على زوجته
Haki Za Mume Juu Ya Mke

بسم لله الرحمن الرحي
Waja wa Allaah! Ninawausia baada ya kuiusia nafsi yangu kumcha Allaah, ndiyo zawadi yetu ya kukutana na Allaah.Anasema Allaah (Ta´ala):
وَتَزَوَّدُواْ فَإِنَّ خَيْرَ الزَّادِ التَّقْوَى وَاتَّقُونِ يَا أُوْلِي الأَلْبَابِ
“Na jitengezeeni zawadi. Na hakika bora yazawadi ni ucha Mungu. Na nicheni Mimi, enyi wenye akili!” (02:197)
Na anasema Mtume ( :( صلى لله عليه وسلم
"Muogope Allaah popote ulipo, na lifutishe ovu [baya] kwa jema, na tangamana na watu kwa tabia zilizo njema."
Waja wa Allaah! Nifuateni tuzungumzie haki hizi zenye baraka, haki za ndoa
ambazo zimekuja katika Kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume ( صلى لله عليه
وسلم ). Ambazo lau kila mmoja katika mwanandoa angezitekeleza wangeliishi
katika upendo, rahmah, mawada na saada.
Mizozo ilioko kwa wanandoa wengi, chanzo ni kuwa mbali na Shari´ah ya Allaah (´Azza wa Jalla), pamoja na kuiga kichwa mchunga makafiri mulhid wa magharibi.
Waja wa Allaah! Hakika haki za kindoa zimegawanyika aina tatu: 1- Haki ambazo ni wajibu kwa mume juu ya mke wake. 2- Haki ambazo ni wajibu kwa mke juu ya mume wake. 3- Na haki ambazo wanashirikiana wote.
Haki ambazo wanashirikiana baina yao. Ya kwanza Kule kuwa halali maisha yao ya kindoa, na uhalali huu wanashirikiana baina yao. Yanakuwa halali ya mume kwa mkewe ambayo si halali kwa yeyote. Na hii ni haki ya wanandoa, na watakiwa kushirikiana wote kwa kuwa mmoja tu hawezi kumfaidikisha mwengine bila ya mwenzake. Ya pili ni kuharamishwa "muswaaharah", yaani mke wake anaharamika kwa mahram wote wa mume kama jinsi ni haramu kwa mama yake, mabanati zake na mahram wake wengine wote.
Tano ni kuishi kwa wema, ni wajibu kwa kila mmoja kuishi na mwenziwe kwa wema ili waishi kwa upendo na mahaba. Anasema Allaah (Jalla wa ´Alaa) katika Kitabu Chake Kitufukufu.
وَعَاشِرُوھُنَّ بِالْمَعْرُوفِ
“Na kaeni nao kwa wema.” (04:19)
وَلَھُنَّ مِثْلُ الَّذِي عَلَيْھِنَّ بِالْمَعْرُوفِ وَلِلرِّجَالِ عَلَيْھِنَّ دَرَجَةٌ
“Nao wanawake wanayo haki kwa Shari´aa kama ile haki iliyo juu yao. Na wanaume wana daraja zaidi kuliko wao.” (02:228)
Jambo la sita wawe na uaminifu kwa kila mmoja kwa mwenziwe, iwe kila mmoja anamuamini mwenziwe. Na wala asimuwekee mmoja mwenziwe shaka katika ukweli wake, nusra yake na ikhaasw yake. Na hilo kutokana na Kauli Yake Allaah (Ta´ala):
إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ
“Hakika Waumini ni ndugu.” (49:10)
Na kwa kauli ya Mtume ( :( صلى لله عليه وسلم
"Hatoamini mmoja wenu mpaka ampendee ndugu yake anachojipendea mwenyewe."
Ama haki za mume juu ya mke wake, kwanza ni kumtii kwa yasiyokuwa
maasi kwa Allaah na Mtume Wake. Amtii mume kwa kutimiza faradhi za dini
na kumtii Allaah (´Azza wa Jalla).Kutoka kwa Abu Hurayrah (radhiya
Allaahu ´anhu) anasema kasema Mtume ( :( صلى لله عليه وسلم
“Atakaposwali mwanamke Swalah zake tano; na akafunga mwezi wake [Ramadhaan]; na akahifadhi sehemu zake za siri; na akamtii mume wake; ataingia katika mlango wowote autakao katika milango ya Jannah.”
Na kutoka kwa ´Abdur-Rahmaan bin ´Awf (radhiya Allaahu ´anhu) anasema,
kasema Mtume ( :( صلى لله عليه وسلم
“Atakaposwali mwanamke Swalah zake tano; na akafunga mwezi wake [Ramadhaan]; na akahifadhi sehemu zake za siri; na akamtii mume wake; ataambiwa [Siku ya Qiyaamah]: Ingia Jannah kupitia mlango wowote uutakao katika milango ya Jannah.”
Kapokea Tirmidhiy kutoka kwa Abu Hurayrah (radhiya Allaahu
´anhu)anasema, kasema Mtume ( :( صلى لله عليه وسلم
"Lau ningeweza kumuamrisha yeyote kumsujudia mwenziwe, ningelimua- mrisha mwanamke kumsujudia mume wake."
Kapokea Tirmidhiy kutoka kwa Ummu Salamah (radhiya Allaahu ´anha)
anasema, kasema Mtume wa Allaah ( :( صلى لله عليه وسلم
"Mwanamke yeyote akifa na mume wake yuko radhi naye, ataingia Peponi."
Angalia ewe dada wa Kiislamu, wewe uko wapi na mume wako?! Hakika yeye [ima] ndio Pepo yako au Moto wako.
Na kutoka kwa Husayn bin Muhsin kuwa ami yake alimwendea Mtume ( صلى
لله عليه وسلم ) kunako haja yake, akamaliza haja yake. Mtume ( ( صلى لله عليه وسلم
akamuuliza, je wewe una mume? Akasema "ndiyo". Akamwambia "Uko vipi
naye?" Akasema "Namfanyia kila kitu ila tu yale nisiyo yaweza."
Akamwambia [Mtume] "Angalia uko naye vipi, kwani hakika yeye [mumeo]
ndiyo Pepo yako na Moto wako."
Na katika haki kubwa ambayo ni wajibu kwa mke, ni yeye kumtii mume wake katika wakati wowote aupendao na autakao. Haki ya mume kitandani. Akimkatalia mume wake bila ya sababu ya Kishari´ah basi kafanya dhambi kubwa katika madhambi makubwa. Lakini iwe kwa sababu ya Kishari´ah. Kama mume kumwita mke wake kitandani [wafanye jimai] naye yuko na hedhi akamwambia [mke] "hapana!". Kwa kuwa haya ni maasi.
"Hakuna utiifu kwa kiumbe katika kumuasi Muumba."
Ama mume wake akimuhitajia bila ya kufanya naye jimai kwenye tupu,
hakuna ubaya wala neno kama alivyokuwa akifanya Mtume wa Allaah ( صلى
لله عليه وسلم ) na wake zake. Mke akimkatalia mume wake kwa sababu moja au
nyingine kama kumletea mume akihitajiacho na kutaka, atakuwa ni mwenye
kumuasi Allaah (´Azza wa Jalla). Amefanya dhambi kubwa katika madhambi
makubwa. Sikiliza kauli ya Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) kasema:
"Naapa kwa Yule ambaye nafsi Yangu iko Mkononi Mwake, hakuna mwanaume amwitae mke wake kitandani akamkatalia isipokuwa yule Aliyeko mbinguni humkasirikia [mke] mpaka atapomridhia [mume]."
Mola (´Azza wa Jalla) Humkasirikia mpaka pale mume wake
atapomridhia.Na kutoka kwa Abu Hurayrah (radhiya Allaahu ´anhu)
anasema, kasema Mtume wa Allaah ( :( صلى لله عليه وسلم
“Mume atakapomwita mkewe kwenye kitanda chake [kwa tendo la ndoa] na yule mke akakataa kumuitika, akamkasirikia mume, Malaika humlaani mpaka kupambazuke.”
Allaahu musta´aan. Je, mwanamke kweli muumini mwenye heshima zake anaweza kuwa radhi kwa hilo?! Na ni ukubwa ulioje wanaolaaniwa kutokana na hali zao?! Allaah Atulinde.
Katika haki za mume juu ya mke wake, ni kumheshimu na kumlindia hadhi yake na kumchungia mali yake na watoto wake na kazi zilizobaki za nyumbani. Kutokana na Kauli Yake Allaah (Ta´ala):
فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِّلْغَيْبِ بِمَا حَفِظَ للهُّ
“Basi wanawake wema ni wale wenye kutii na wanaojilinda hata katika siri kwa kuwa Allaah Ameamrisha wajilinde.” (04:34)
Na kauli ya Mtume ( :( صلى لله عليه وسلم
"Na mwanamke ni mchungaji wa nyumba ya mume wake na watoto wake."
Na katika haki za mume juu ya mke wake, ni tabia yake [mke] nzuri na adabu
zake. Asimuudhi kwa ulimi wake wala kwa neno baya, na ajiweke mbali na
kila kitachomuondolea hadhi na haya yake. Nisikilize vizuri ewe dada wa
Kiislamu kauli ya Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) kama ilivyo katika Hadiyth
swahiyh iliopokelewa na Tirmidhiy na ibn Hibbaan katika Hadiyth ya Abu
Darda (radhiya Allaahu ´anhu)anasema, kuwa Mtume ( ( صلى لله عليه وسلم
kasema:
"Hakuna kitu chenye uzito kwenye mizani ya muumini siku ya Qiyaamah kama tabia njema."
Nnatumai asijekudhani yeyote kuwa maneno haya ni kwa mke tu, bali hata mume pia.
Katika Hadiyth swahiyh iliopokelewa na Ahmad na ibn Hibbaan na Bazzar,
katika Hadiyth ya Abu Hurayrah (radhiya Allaahu ´anhu) anasema, aliulizwa
Mtume wa Allaah ( :( صلى لله عليه وسلم
"Kitu gani kitachowafanya wengi kuingia Peponi, akasema ni "taqwa Allaah" [kumcha Allaah] na tabia njema."Na ni kipi kitachowafanya wengi kuingia Motoni? Akasema "Ni mdomo na tupu."
Ndimi na tupu, ni juu ya mke kuhifadhi sauti yake na kuzuia mikono yake kutokana na maovu, pia kwa watoto wake au ndugu zake.
Na katika haki za mume juu ya mke wake, ni kushikama [kubaki] kwenye nyumba ya mume wake. Asitoke ila kwa idhini yake na ridha yake na kuchunga jicho lake atapotoka na asitoke kwa kujishauwa. Anasema Allaah (Ta´ala):
وَقَرْنَ فِي بُيُوتِكُنَّ وَلَا تَبَرَّجْنَ تَبَرُّجَ الْجَاھِلِيَّةِ الْأُولَى
“Na kaeni majumbani kwenu, wala msijishauwe kwa majishauwo ya kijahilia ya kizamani.” (33:33)
Na Anasema Allaah (Ta´ala):
وَقُل لِّلْمُؤْمِنَاتِ يَغْضُضْنَ مِنْ أَبْصَارِھِنَّ وَيَحْفَظْنَ فُرُوجَھُنَّ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَھُنَّ إِلَّا مَا ظَھَرَ مِنْھَا
Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao, wala wasionyeshe uzuri wao isipokuwa unaodhihirika. (24:31)
Na katika haki za mume juu ya mke wake, ajitengeneze na kujipamba. Katika haki kubwa ni kumuona mume mke wake akiwa mzuri.
Na mimi namnasihi kila mke kutokana na harufu mbaya sawa ya mwili au nguo. Katika mambo yanayo udhi ni kumuonamwanamke kabla ya kutoka nyumba kwenda sehemu mbali mbali za kijinga anajipamba na kujipendezesha, anabaki huko masaa na masaa ili watu wamuone ni mzuri. Anajipamba na kujipendezesha kisha anatoka barabarani. Kisha mume anapokuja kukaa naye na nguo alizoshinda nazo zenye harufu mbaya. Mume kutokana na fitrah yake, hukimbia kutokana na harufu mbaya.
Na hili linamuhusu mume pia, hata mume pia anatakiwa kujipamba na kujipendezesha kwa ajili ya mke wake. Anasema ibn ´Abbaas (radhiya Allaahu ´anhuma):
"Mimi napenda kumpambia mke wangu kama [yeye] anavyopenda kunipambia mimi."
Mwanaume pia ajipambe kwa mke wake, anukie harufu nzuri kama alivyosema ibn´Abbaas (radhiya Allaahu ´anhuma):
"Mimi napenda kumpambia mke wangu kama [yeye] anavyopenda kunipambia mimi."
Na imekuja katika Hadiyth swahiyh kutoka kwa Mtume ( ( صلى لله عليه وسلم
kasema:
"Hakika Allaah ni Jamiyl [Mzuri] na Anapenda vizuri."
Allaah ni Mzuri na Anapenda vizuri. Tahadhari kujipamba kwa mapambo ya haramu; kama kuchonga meno, kuunganisha nywele na mfano wa hayo. Haijuzu kwake mwanamke kuunganisha nywele zake kwa nywele zingine na hili ni haramu.
Na katika mapambo haramu pia ni mwanamke [wa Kiislamu] kujifananisha na mwanamke wa kikafiri katikamapambo yao na kufuata kipotofu. Hali kadhalika rangi ya kucha, na hili linazuia ufikaji wa maji. Akijipaka nayo mwanamke na akatawadha kisha akaswali wudhuu wake na swalah yake ni batili kwa kuwa maji hayakuufikia mwili.