Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, October 19, 2013

Rais Uhuru Kenyatta kutohudhuria vikao ICC


Rais Uhuru Kenyatta kutohudhuria vikao ICCMahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC imechukua uamuzi wa kumsamehe Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya asihudhurie vikao vya kesi inayomkabili huko Hague nchini Uholanzi. Taarifa iliyotolewa jana na mahakama hiyo imeeleza kuwa, Rais Kenyatta atahudhuria kikao cha ufunguzi wa kusikiliza kesi yake na kikao cha mwisho cha kutolewa hukumu ya kesi inayomkabili. Awali, Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ilimtaka Rais Kenyatta ahudhurie mwenyewe kwenye kwenye vikao vyote ya kesi inayomkabili, ambayo imepangwa kuanza kusikilizwa tarehe 12 Novemba mwaka huu. Hivi karibuni, Umoja wa Afrika uliitaka Mahakama ya Kimataifa ya Jinai kusitisha zoezi la kusikiliza kesi za Rais Kenyatta na Naibu wake William Ruto, hadi pale viongozi hao watakapoondoka madarakani. Viongozi hao wa Kenya wanatuhumiwa kwa kufanya uchochezi na kusababisha mauaji ya watu wasiopungua 1,500 katika machafuko yaliyojiri Kenya mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007.