Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, October 9, 2013

Waliokufa kwenye ghasia Sudan ni 70


Waliokufa kwenye ghasia Sudan ni 70Afisa wa serikali ya Sudan ametangaza kuwa, idadi ya watu waliouawa katika machafuko ya hivi karibuni mjini Khartoum yaliyoanza wakati wa maandamano Septemba 23 ni 70. Abdurahman al Khadr Gavana wa jiji la Khartoum ameongeza kuwa idadi hiyo imethibitishwa na Wizara ya Afya ya nchi hiyo na kwamba uchunguzi zaidi unafanywa ili kufahamu sababu kuu zilizosababisha machafuko hayo.
Maandamano yalianza nchini Sudan baada ya bei ya mafuta ya petroli kupanda karibu mara dufu. Nchi hiyo ilipoteza mabilioni ya dola baada ya Sudan Kusini kujitenda mwaka 2011, na inasemekana kuwa tangu wakati huo serikali ya Khartoum imekuwa ikikabiliwa na mfumoko wa bei, kuanguka thamani ya sarafu na kupungua akiba ya pato la kigeni.
HII NDIO TAARIFA YA POLISI KUHUSU VIJANA WALIOKAMATWA WAKIFANYA ZOEZI POLINI HUKO MTWARA Written By umar makoo on Wednesday, October 9, 2013 | 4:42 AM 45 3 1 Hizi ni moja ya CD zilizokamatwa na askari wa jeshi la polisi Mtwara ikiwemo na kuwakamata vijana 11 ambao wanadaiwa walikua wakifanya mazoezi ya kijeshi waliyokua wakijifunza kutoka kwenye CD za magaidi zilizokua na mafunzo kutoka kwa makundi ya Al Shabaab na Al Qaeda. Taarifa zaidi unaweza kuzisoma hapo chini kwenye hiyo taarifa iliyotolewa na jeshi la polisi. 2

Original from: http://www.googlehabari.blogspot.com/2013/10/hii-ndio-taarifa-ya-polisi-kuhusu.html
Copyright EXEIdeas - All Ri