Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, October 2, 2013

Mufti wa Oman ataka mshikamano wa Waislamu


Mufti wa Oman ataka mshikamano wa Waislamu
Mufti wa Oman amesema kuwa umma wa Kiislamu unapaswa kuwa na urafiki, upendo na amani kuliko nyuma nyinginezo, kwani  huo ndio ujumbe wa umma huu. Akizungumza na vyombo vya habari  pamoja na mwenyeji wake Ayatullah Muhsin Araqi Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kuyakurubisha Pamoja Madhehebu za Kiislamu  mjini Tehran, Sheikh Ahmad bin Hamad al Khalili amesema kuwa, umma wa Kiislamu unapita katika kipindi nyeti mno na kusisitiza  kuwa, hivi sasa umma huo  unahitajia kurejea haraka kwenye umoja na mshikamano. Akielezea mazungumzo yake aliyoyafanya na viongozi wa kidini hapa nchini, Mufti Sheikh al Khalili wa Oman amesema kuwa, maulamaa wakubwa wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wametoa mapendekezo kadhaa ambayo yanahitajia kushughulikiwa kivitendo. Ameongeza kuwa, mapendekezo hayo yanahitaji kuwekewa mikakati na hata kuundwa kamati za kuyashughulikia ipasavyo. Mufti wa Oman amesisitiza kuwa, kuna ulazima wa kufanyika mazungumzo hata kama na wapinzani kwa lengo la kuondoa hitilafu zilizopo, kwani mazungumzo ndio njia pekee inayoweza kumkinaisha mwanadamu na hatimaye kufuata njia ya saada.