Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, October 8, 2013

Watoto 362 wafariki kutokana na lishe duni Niger


Watoto 362 wafariki kutokana na lishe duni Niger
Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, watoto 362 walio chini ya umri wa miaka mitano wamefariki dunia kutokana na lishe duni nchini Niger. Taarifa ya Umoja wa Mataifa imeeleza kuwa, watoto hao wamefariki dunia katika eneo la Zinder mashariki mwa Niger kati ya mwezi Januari hadi Septemba mwaka huu. Taarifa hiyo imeeleza kuwa, asilimia 90 ya vifo katika maeneo ya Zinder, Magaria na Mirriah inatokana na lishe duni kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano. Zinder ni mji wa pili kwa wingi wa watu nchini Niger, na eneo hilo hukabiliwa mara kwa mara na ukosefu wa chakula unaosababishwa na ukame, huku watoto na wanawake wakiwa wahanga wakubwa wa balaa hilo.