Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, October 9, 2013

Mhadhiri Saudia ahukumiwa kwa kumnajisi binti yake


Mhadhiri Saudia ahukumiwa kwa kumnajisi binti yake
Mhadhiri mmoja wa kidini nchini Saudi Arabia amehukumiwa kifungo cha miaka minane jela na kuchapwa viboko 800 kwa kosa la kumnajisi bintiye mdogo wa miaka mitano na kumtesa hadi kufariki dunia. Mahakama ya Saudi Arabia Jumatatu hii ilimuamuru Fayhan al Ghamdi kumlipa mke wake wa zamani yaani mama wa binti huyo fedha za diya ya damu dola za Kimarekani 270,000. Mke wa pili wa mahdhiri huyo aliyekutwa na hatia ambaye naye ameshtakiwa kwa kushiriki kwenye jinai hiyo amehukumiwa kifungo cha miezi kumi jela na viboko 150. Binti huyo wa Saudia aliyekuwa na umri wa miaka mitano alilazwa hospitali mwezi Disemba mwaka juzi akiwa na majeraha kadhaa, michubuko, majeraha ya kuungua moto na kupasuka fuvu la kichwa. Wanaharakati nchini Saudi Arabia na wa nchi za nje wamelaani vikali jinai hiyo iliyofanywa na baba huyo kwa bintiye na kuitaja adhabu iliyotolewa na mahakama ya nchi hiyo kwa mtenda jinai huyo kuwa ya kiwango cha chini mno. Wanaharakati hao wamesema mtenda jinai huyo alipaswa kufungwa jela maisha au kunyongwa ili iwe mfano kwa wengine.