Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 14, 2013

Walowezi wa Israel wavamia Msikiti wa al Aqswa


Walowezi wa Israel wavamia Msikiti wa al Aqswa
Makumi ya walowezi wa Kizayuni wenye misimamo ya kufurutu ada wamevamia Msikiti Mtukufu wa al Aqswa huko mashariki mwa Quds na kupeperusha bendera za Israel ndani ya msikiti huo.
Ripoti zinasema kuwa, tukio hilo limejiri leo na baada ya hapo polisi ya Israel ilifunga mlango wa Magharba unaotumiwa na wageni kuingia ndani ya msikiti huo mtukufu.
Tukio kama hilo pia lilishuhudiwa Septemba 18, ambapo askari wa utawala ghasibu wa Israel waliva uwanja wa msikiti huo na kuwapulizia gesi za kutoa machozi waumuni wa Kipalestina.
Msikiti wa al Aqswa uliopo katike mji wa al Quds unaokaliwa kwa mabavu na Israel umekuwa kitovu cha vurugu na machafuko. Mayahudi wanataka kubomoa msikiti huo ambao ni kibla cha kwanza cha Waislamu kwa kisingizio cha kutafuta mabaki ya hekalu la Nabii Sulaiman.