Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, October 30, 2013

Wataka sheria ya maandamano irekebishwe Misri


Wataka sheria ya maandamano irekebishwe MisriKituo cha kitaifa cha kutetea haki za biandamu cha Misri kimetaka sheria inayohusu maandamano ifanyiwe marekebisho. Kituo hicho kimeeeleza kuwa, katika rasimu ya katiba kuna baadhi ya vipengee vinavyobana haki ya wananchi ya kuandamana kwa amani. Kituo hicho cha kutetea haki za binadamu cha Misri kimesema, utangulizi wa katiba unapaswa kutambua haki isiyopingika ya kuandamana wananchi, na kwamba wananchi wanaweza kueleza malalamiko yao bila kizuizi chchote kwa maandamano ya amani.
Sheria ya maandamano katika rasimu ya katiba ya Misri inaeleza kuwa, ni marufuku waandamanaji kukaribia maeneo ya serikali na kidiplomasia, maafisa wa usalama wanapaswa kuarifiwa juu ya maandamano kabla ya maasaa 24 na hakuna haki ya kukusanyika katika meidani na kufunga barabara.