Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, October 12, 2013

Dola milioni 500, pato la M23 kwa magendo ya madini


Dola milioni 500, pato la M23 kwa magendo ya madini
Gazeti la Los Angeles Times linalochapishwa nchini Marekani limeandika kuwa waasi wa M23 walioko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hujipatia takribani dola milioni 500 kila mwaka kutokana na magendo ya dhahabu nchini humo. Uchunguzi uliofanywa na taasisi ya  kutetea haki za binadamu ya Enough ya Washington nchini Marekani unaonyesha kuwa, waasi wa M23 waliojizatiti mashariki mwa nchi hiyo hufanya magendo ya madini ya dhahabu na kujipatia mamilioni ya dola kila mwaka, pesa ambazo hutumiwa kununulia silaha na kufanya jinai na mauaji ya halaiki katika  eneo hilo. Taasisi hiyo imeeleza kuwa, licha ya kinara wa kundi hilo Bosco Ntaganda kupelekwa kwenye mahakama ya ICC kwa tuhuma za kutenda jinai za kivita, lakini wasaidizi wake wamefanikiwa kutorosha kwa njia za magendo dhahabu za Kongo na kuziuza nchini Imarati, kupitia nchi jirani za Burundi na Uganda. Uchunguzi huo umeeleza kuwa, kila mwaka tani 12 za magendo ya madini ya dhahabu yenye thamani ya dola milioni 500 hupelekwa nje ya nchi hiyo kinyume cha sheria.