Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 21, 2013

41 wauliwa katika mashambulizi Sudan Kusini


41 wauliwa katika mashambulizi Sudan Kusini Watu wasiopungua 41 wameuawa na wengine 63 kujeruhiwa katika mashambulizi ya silaha yaliyotekelezwa katika jimbo la Jonglei mashariki mwa Sudan Kusini. Ripoti za awali zinaeleza kuwa watu 41 wameuawa na wengine 63 kujeruhiwa, huku hali ya baadhi ya majeruhi zikiwa mbaya sana. Hussein Maar Kaimu gavana wa jimbo la Jonglei amesema kuwa kuna uwezekano wa baadhi ya majeruhi ambao hali zao ni mbaya sana wakaaga dunia wakati wowote. Maar ameongeza kuwa wavamizi walikuwa na silaha za otomatiki na kwamba waliiba maelfu ya ng'ombe kwenye shambulizi hilo. Kaimu gavana wa jimbo la Jonglei ambalo ni jimbo kubwa zaidi huko Sudan Kusini amesema kuwa wanamgambo wanaoongozwa na David Yau Yau wanashukiwa kuhusika na shambulio hilo.