Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, October 2, 2013

Wazayuni waendelea na maneva ya kijeshi Palestina


Wazayuni waendelea na maneva ya kijeshi Palestina
Utawala wa Kizayuni wa Israel umeendelea kwa siku ya pili mfululizo kufanya maneva ya kijeshi katika eneo la kaskazini mwa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu. Taarifa zinasema kuwa,  kikosi cha ardhini cha jeshi la Israel ambacho tokea jana kilianza kufanya maneva na luteka hiyo ya kijeshi katika eneo linalopakana na nchi tatu za Syria, Lebanon na Palestina inayokaliwa kwa mabavu, yameendelea tena leo kwa kutumia silaha mbalimbali, zikiwemo silaha  nzitonzito. Taarifa zinasema kuwa, milio ya milipuko ilisikika pia karibu na maeneo yanayopakana na mashamba ya Shaba'a nchini Lebanon. Taarifa hizo zimeelza kuwa, ndege ya kijasusi ya utawala wa Israel pia imekiuka sheria za kimataifa kwa kuingia kwenye anga ya maeneo ya kusini mwa Lebanon.