Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, October 6, 2013

BABA NA WANAWE WAWILI WAPIGWA RISASI WAKITOKA KUSALI MSIKITINI


Watu watatu inaoaminika ni baba na wanawe wawili wamepigwa risasi wakati wanatoka kusali swala ya ijumaa
katika msikiti wa Villiers-le-Bel commune, kaskazini mwa jiji
la paris kilomita 17.4 kutoka katikati ya mji huo, limeripoti gazeti la lugha ya kifaransa la La Parisien.
 

Uchunguzi wa awali unaonesha kwamba risasi nne ziliwapata watu hao na mshambulizii wa tukio hilo alifanikiwa kukimbia eneo la bila kujulikana.
 

Baba na mmoja wa watoto wake walijeruhiwa vibaya
kwa risasi na walikimbizwa katika hospitali ya Beaujon huko Clichy ambapo mwanawe mwingine alijeruhiwa kidogo na kupelekwa Hospitali ya jirani ya Gonesse commune kilomita moja na nusu toka msikitini hapo.

 
Polisi wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na bado wanamtafuta mshambulizi huyo.

 
Kwa miaka ya karibuni waislamu katika nchi za Ulaya wamekuwa katika kipindi kigumu cha kunyanyaswa, kupigwa, kuuliwa pamoja na kubaguliwa.


polisi wakiwa katika tukio hilo