Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, October 8, 2013

Rwanda yatakiwa iache kuwasaidia waasi Kongo DRC


Rwanda yatakiwa iache kuwasaidia waasi  Kongo DRC
Marekani imeitaka serikali ya Rwanda kutoa ushirikiano utakaosaidia kukomeshwa mapigano huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Samantha Power, mwakilishi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, Rwanda ikiwa ni nchi jirani na Kongo inapaswa kuwa na nafasi ya moja kwa moja katika mchakato wa kuleta amani na utulivu nchini Kongo. Bi. Power amesisitiza kwamba nchi zote za eneo la Maziwa Makuu ya Afrika zinapaswa kufanya juhudi maradufu za kuwatokomeza waasi walioko mashariki mwa nchi hiyo. Hapo jana ujumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa uliyataka makundi ya waasi mashariki mwa Kongo kuacha kuendeleza machafuko katika eneo hilo. Inafaa kuashiria hapa kuwa, mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Kongo na waasi wa M23 kwa upatanishi wa Uganda bado yanaendelea, lakini hadi sasa hayajakuwa na natija yoyote ile.