Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, October 8, 2013

Kenya kutoa zawadi kwa wafichuaji wa Westgate


Kenya kutoa zawadi kwa wafichuaji wa Westgate
Polisi ya Kenya imetangaza kuwa iko tayari kutoa kitita cha shilingi laki tano za nchi hiyo ambazo ni sawa na dola 5, 827 kwa mtu atakayetoa taarifa zitakazosaidia kukamatwa mwenye gari linalosadikiwa kutegwa  mabomu kwenye shambulio lililofanywa zaidi ya wiki mbili zilizopita kwenye jumba la biashara la Westgate jijini Nairobi, Kenya.  Mkuu wa kikosi  maalumu cha kupambana na ugaidi nchini Kenya ameeleza kuwa, gari hilo linashukiwa  lilikuwa limesheheni mada za milipuko na silaha na kuongeza kuwa kikosi hicho bado kinaendelea kumsaka mmiliki wa gari hilo.  Amesema kuwa, awali mmiliki wa gari hilo alikuwa Mkenya mwenye asili ya Kisomali. Kundi la al Shabab la nchini Somalia lilitangaza kuhusika na shambulio hilo lililopelekea watu wasiopungua 67 kuuawa ingawa hadi sasa watu wengine 39 waliokuwepo kwenye eneo hilo hawajulikani walipo. Kundi la al Shabab limeitaka serikali ya Kenya kuondoa majeshi yake nchini Somalia, kinyume cha hivyo itakabiliwa na mashambulio mengine kwenye maeneo nyeti ya nchi hiyo. Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesikika akisema kuwa, serikali ya Nairobi haitayaondoa majeshi yake nchini Somalia hadi pale  hali ya amani na utulivu itakaporejea nchini humo.