Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 14, 2013

Sudan kuimarisha usalama eneo la Darfur Mashariki


Sudan kuimarisha usalama eneo la Darfur Mashariki
Jeshi la Sudan limepeleka askari zaidi huko Mashariki mwa eneo la Darfur kwa lengo la kuimarisha usalama zaidi wa raia wakati huu wa sikukuu ya Idil Adha. 
Bilal Saed Daqis ambaye ni miongoni mwa maafisa wa Darfur amesema kuwa, wanajeshi zaidi wamepelekwa mashariki mwa eneo hilo ili kuzuia machafuko kati ya makabila ya al Manaliya na ar Razqat na kuimarisha usalama zaidi.
Wakati hayo yanaripotiwa askari watatu wa kikosi cha kulinda amani wa Umoja wa Mataifa UNAMID wanaotoka Senegal wameuawa katika shambulio lililofanywa dhidi ya msafara wa umoja huko kwenye eneo la Darfur. Mwakilishi maalumu wa kikosi cha UNAMID Mohamed Ibn Chambas amesema kwamba, shambulizi hilo ni jinai na kwamba serikali ya Sudan inapaswa kuchukua hatua muhimu ili kuzuia mashambulizi kama hayo.