Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 7, 2013

PICHA:DALADALA LILILOBEBA WANAFUNZI LAPATA AJALI MBAYA,WANAFUNZI WANUSURIKA


 Askari wa usalama barabarani wakijipanga kutoa huduma baada ya basi la daladala lililokuwa limebeba wanafunzi takriban 50 wa shule ya msingi ya Mgulani kugongana na gari dogo aina ya RAV 4 na kupinduka katika makutano ya Kenyatta Avenue na Barabara ya Ali Hassan Mwinyi jijini Dar es salaam jana  jioni.

 Dereva wa gari dogo akiwa na mtoto wa umri wa takriban miaka mitatu walijeruhiwa vibaya na kukimbizwa hospitali. Wanafunzi wote walinusurika.
 Uharibifu wa miundumbinu baada ya ajali hiyo
 Askari wa usalama barabarani wakiondoa mabegi ya wanafunzi hao ambao walitafutiwa basi lingine kuwapeleka hospitali kwa uchunguzi zaidi
 Wanafunzi wakiwa katika gari walilotafutiwa baada ya ajali hiyo
 Magari ya break-down yakifanya juhudi ya kunyanyua basi hilo