Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, October 4, 2013

Wamarekani walalamikia likizo zisizo na malipo


Wamarekani walalamikia likizo zisizo na malipo
Wafanyakazi wasiopungua milioni moja wa serikali ya shirikisho ya Marekani wamelalamikia hatua ya nchi hiyo ya kuwapa likizo bila ya mishahara yao. Taarifa zinasema kuwa, wafanyakazi hao wamelalamikia vikali hatua ya kuendelea kubaki  nyumbani kwa siku ya nne mfululizo bila ya kulipwa mishahara yao na wanataka warejeshwe kazini haraka iwezekanavyo. Fikra za walio wengi na wafanyakazi nchini humo wanajihesabu kuwa ni mateka na wahanga wa mivutano ya kisiasa ndani ya Baraza la Kongresi. Hapo jana, Rais Barack Obama wa Marekani alisisitiza kuwa kuendelea kusimamishwa idara za shirikisho ni pigo kubwa kwa nchi na uchumi wa Marekani. Taarifa zinasema kuwa, thuluthi mbili ya wafanyakazi wa serikali akiwemo Obama mwenyewe, watalazimika kufanya kazi bila ya malipo hadi mgogoro wa bajeti kati ya Warepublican na Wademokrat utakapotatuliwa. Wademokrat na Warepublican wanazozana juu ya miswada iliyopendekezwa  na serikali ya Obama juu ya marekebisho ya bima ya afya.