Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, October 21, 2013

Amnesty yakosoa ukiukaji haki za binadamu Saudia


Amnesty yakosoa ukiukaji haki za binadamu  Saudia
Shirika la Msamaha Duniani (Amnesty International) limeikosoa Saudi Arabia kwa kutokomesha hali ya kutisha ya haki za binadamu nchini humo. Amnesty International imetoa ripoti iliyoiwasilisha kwa Umoja wa Mataifa ikibainisha ukandamizaji na uvunjaji wa haki za binadamu dhidi ya raia wa Saudi Arabia kama vile kutiwa mbaroni  na kushikiliwa kiholela, kukatiwa hukumu zisizo za kiadilifu na mateso mengine katika kipindi cha miaka iliyopita. Amnesty International imewasilisha ripoti yake hiyo kwa Umoja wa Mataifa kuhusu uvunjaji wa haki za binadamu nchini Saudia Arabia kabla ya kuanza mkutano wa umoja huo uliopangwa kufanyika hii leo Jumatatu huko Geneva Uswisi, kuchunguza hali ya haki za binadamu huko Saudia. Ukandamizaji mwingine uliotajwa kwenye ripoti hiyo ni kuhusu wimbi jipya la ukandamizaji dhidi ya wananchi huko Saudi Arabia katika kipindi cha miaka miwili ya hivi karibuni.