Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, October 6, 2013

Magaidi waendelea kumwaga damu za raia nchini Iraq


Magaidi waendelea kumwaga damu za raia nchini Iraq
Wafanya ziara wasiopungua watano wameuliwa leo na wengine wasiopungua 17 wamejeruhiwa katika eneo la Qahira kaskazini mwa mji mkuu wa Iraq, Baghdad baada ya gaidi mmoja kujiripua ndani ya msafara wa wafanya ziara hao waliokuwa wakielekea kwenye haram ya Imam Muhammad Al- Jawad AS kuomboleza siku aliyouliwa shahidi Imamu huyo wa tisa wa Waislamu wa madhehebu ya Shia. Wakati huohuo wanafunzi 14 pamoja na mwalimu wao mkuu wameuliwa katika shambulio jengine la kigaidi lililofanywa leo pia ndani ya uwanja wa shule moja ya msingi huko kaskazini mwa Iraq. Lori lililosheheni mada za miripuko liliingizwa na kuripuka ndani ya uwanja wa kuchezea watoto wa shule moja ya msingi katika mji wa Tel Afar ulioko kilomita 70 kaskazini magharibi mwa wa Mosul na kusababisha vifo vya watoto hao pamoja na mwalimu wao mkuu. Zaidi ya watu elfu sita wameuawa nchini Iraq tangu ulipoanza mwaka huu wa 2013, elfu moja kati yao wakiwa wamepoteza maisha katika mashambulio ya kigaidi yaliyofanywa nchini humo ndani ya kipindi cha mwezi mmoja tu uliopita wa Septemba. Hapo jana watu wasiopungua 60 waliuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa katika milipuko miwili iliyolenga Waislamu wa madhehebu ya Shia waliokuwa wakienda kuzuru haram tukufu ya Imam Jawad AS katika viunga vya mji mkuu wa Iraq, Baghdad.