Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, October 8, 2013

UN na AU kujadili mgogoro wa Sudan Mbili


UN na AU kujadili mgogoro wa Sudan Mbili
Wawakilishi kutoka Umoja wa Afrika  na  wale wa Umoja wa Mataifa watakutana leo Addis Ababa mji mkuu wa Ethiopia kwenye kikao cha kila mwaka, ambapo mwaka huu ajenda kuu itakuwa ni kuujadili kwa kina mgogoro wa  mpaka kati ya nchi za Sudan na Sudan Kusini. Taarifa iliyotolewa na Umoja wa Afrika imeeleza kuwa, licha ya mgogoro wa Sudan mbili,  wajumbe wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika watajadili pia hali ya mambo katika eneo la Maziwa Makuu ya Afrika, Pembe ya Afrika, Jamhuri ya Afrika ya Kati na eneo la Sahel. Sudan Kusini ambayo awali ilikuwa sehemu ya Sudan, ilijitangazia uhuru wake mwezi Juni 2011. Hata hivyo, nchi hizo mbili zimetumbukia kwenye mgogoro mkubwa baada ya kila upande kudai haki ya umiliki wa maeneo matano ya mpakani na hali kadhalika tuhuma za kila upande za kuwaunga mkono waasi wa upande wa pili. Hadi sasa, Sudan imeshaishitaki Sudan Kusini mara tano kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kuwaunga mkono wapinzani wa serikali ya Khartoum.