Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, October 12, 2013

AU: ICC isiwashtaki viongozi walioko madarakani


AU: ICC isiwashtaki viongozi walioko madarakaniViongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika AU wanaokutana makao makuu ya umoja huo mjini Addis Ababa, Ethiopia wameitaka Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC isiwafungulie mashtaka viongozi wa nchi za Afrika wanapokuweko madarakani. Viongozi hao aidha wameitaka mahakama hiyo iakhirishe kesi za marais wa Uhuru Kenyatta wa Kenya na Omar al Bashir Sudan. Mkuu wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Bi Dlamini Zuma, amesema Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai zinapaswa kuakhirisha haraka usikilizaji wa kesi za viongozi wa Kenya waliochaguliwa na wananchi. "Baraza la Usalama na ICc zinapaswa kushirkiana nasi ili kuwezesha uongozi wa Kenya uliochaguliwa na wananchi uweze kutekeleza majukumu yake ya kikatiba kwa kulizingatia kwa haraka suala la uakhirishaji kesi zinazosikilizwa na ICC dhidi ya Rais na Makamu wa Rais wa Kenya", amesema Zuma. Mbali na Rais, Naibu wa Rais wa Kenya William Ruto naye pia anakabiliwa na kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai yenye makao yake the Hague, Uholanzi ya kuhusika na kuongoza machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu wa Kenya wa mwaka 2007 yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu 1,200…/