Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, October 6, 2013

15 wauawa 85 wajeruhiwa katika machafuko Misri


15 wauawa  85 wajeruhiwa katika machafuko Misri
Watu wasiopungua 15 wameuawa katika machafuko yaliyotokea leo nchini Misri katika maadhimisho ya mwaka wa 40 wa tangu yalipoanza mashambulizi ya Misri dhidi ya vikosi vya utawala wa Kizayuni wa Israel katika vita vya mwaka 1973.
Khaled al Khatib, mmoja wa maafisa wa Wizara ya Afya ya Misri amethibitisha habari hiyo. Saba kati ya watu hao wameuawa katika Medani ya Ramses mjini Cairo. Watu wengine 85 wamejeruhiwa katika machafuko yaliyotokea kwenye maeneo tofauti ya Misri.
Polisi wamewafyatulia risasi na mabomu ya kutoa machozi makundi ya watu waliokuwa wanaandamana huku wengine wakijaribu kuingia kwenye Medani ya Tahrir ambako maelfu ya watu wanaounga mkono jeshi la Misri walikuwa wamekusanyika kuadhimisha siku hiyo.
Huko Delga, kusini mwa Cairo, duru za hospitali zimeliambia shirika la habari la Reuters kwamba polisi walifyatua risasi hai katikati ya kundi la watu waliokuwa wanarusha mawe, na kumuua mtu mmoja.
Watu wengine wameuliwa katika maeneo mengine yaliyoshuhudia machafuko nchini Misri.